RAPCHA Lissa  cover image

Lissa Lyrics

Lissa Lyrics by RAPCHA


Saa sita mchana jua la utosi 
Chuo bomu limetema nimekaa kibosi 
Ata presha ya msosi sina
Somebody is calling oh kumbe Lisa
Nimemsave "Love of my Life"

Nikaweka na loud speaker
Nikamsikia anaongea ka analia
Nikamuuliza are you okay monalisa
Akanianiambia "Babe siko sawa kabisa
Nadaiwa ada na Jumatatu ndo tunaanza paper yani
Na nisipolipa siruhusiwi kufanya mitihani
Laki tano nzima nitaitoa wapi yaani"

Oh don't worry nalifix boo
Kwa kuwa nishadaka hela boom kalibeba hilo jukumu
Kamwabia basi nitakutumia
Usikate simu kwanza love ili uniambie ikiingia
Mmmh baby mbona hii namba ina jina la kiume
'Hio line ni kaka yangu alinisajilia'
Laki tano kwenda kwa Lisa bonyeza moja kuidhibitisha
Mbili kubatilisha mimi nikadhibitisha 
Laki tano na elfu tano na makato ya kutoa
Kwenye account yake pale pale ikadhibitishwa

She was like thanks baby nimeiona
Jioni jua likipoa nitakuja kwako kukuona
And for real nimekumiss kinoma
Nikamwambia nitafurahi sana kama nitakuona

Saa kumi na moja mtoto hajatimba
Labda ndo anatoka home 
Acha nivunge mida mida anafika
Saa moja kamili mtoto hajatimba
Nikasema huenda foleni kuwa ila punde tu atafika
Saa tatu usiku mtoto hajatimba giza limetinga
Nishampigia sana simu hapokei text zinadunda

Nikawaza mpaka usingizi ukanichukua
Siku ya pili, simu hapokei text hajafungua
Siku ya tatu kimya nikasanuka nimcheck beshte yake
Huwezi amini nilijuta kumpigia
Nikamwambia... Hey shem you good? "Am good"
Siku ya tatu beste yako kanilia buyu
Nowadays Lissa mbona ana madrama huyu?
Akaniambia 

"Shem kama una kifua nitakwambia
Kweli Lissa amechange ana bwana mpya msanii
Huyo ndo anamdrive crazy, juzi si ulituma hela
Ada alipokulilia, hiyo hela kampa bwana yake kuitumia"

Dah! Maumivu huwa makali ukimpa kitu mtu umpendaye
Akampatia ampendaye zaidi
Magoti yaliniisha nguvu chozi mbupu ndichi
Roho iliniuma sikufichi

Dah! Nikaondoka home kwa hasira nimfuate Lissa
Cause jealous inanitesa na kila nikimwaza
Naona ka dereva ana utani na mimi
Dala dala inaenda taratibu 
Nilitamani nikaiendeshe mimi
Nikafika mpaka kwa Lissa
Ile nakaribia mlango naskia mziki
Ila kuna sauti ka sizielewi

Nikaona siwezi ngonga mlango
Nikapita nao na teke mpaka ndani
Nilichokiona sitosahau maishani
Kidume kinamkazia kitanda ndani
Ye busy analia, machozi hayatoki anaifinyia ndani
Hata hawakushtuka wamhofia nani?
Jamaa akapiga tako nane akamwagia ndani

Nilipatwa kizunguzungu nusu nianguke sikuweza kuamini
Lissa mbona umenitenda hivi? Nimekukosea nini?
Ungeniambia tuachane ningekuacha huru
Mwisho wa siku ningepona sasa haya yote ya nini?

Lissa kanibadilikia sura mpaka sauti akanichange-ia
Akaanza kunitimua huku na matusi ananishushia
Ye na bwanake wakaanza nipush mpaka nje
Akanipigia kelele "Mwizi" watu wakanijazia
Wote wakanijalia wameshika mawe na marungu
Wakanipiga kama mwizi huu mtaa sina ndugu

"Tunaua, tunaua... Shehe tuwache tushammaliza.."

Hakuna wa kunitetea wakanivika tyre ya gari
Wakawasha moto fasta nikaanza teketea
Maumivu ya moto ndio haya
Waloniumiza moyo wameteketeza mwili vibaya
Nina sekunde chache za kuvuta pumzi ya dunia nzuri
Ilojaa binadamu wengi  wa ubaya

Sawa Lisa nakuwacha ufurahi
Mapenzi niliyokuonyesha umeamua kunitoa uhai
Ahadi tulizoweka zimezimwa na tamaa zako
Mi nakwenda karma itakulipa bye bye 

(Bin Laden)
 

Watch Video

About Lissa

Album : Lissa (Single)
Release Year : 2021
Copyright : (c) 2021
Added By : Huntyr Kelx
Published : Jun 09 , 2021

More lyrics from Wanangu 99 album

More RAPCHA Lyrics

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl