Mauzauza Lyrics by ZUCHU


(Mocco)

Funua usijipe mapana
Eti mwili kujitutumusha
Nitakutawanya 
Ka bahari na fimbo ya Musa

Umejigeuza soji
Si wa Corolla wala Vogi
Na hilo wala kufoji
Eti lina kupa kodi

Oooh leo nikome (Mwenye kiranga)
Hujalijua vizuri litimbwi ni la vanga (Mwenye kiranga)
Oooh leo boda umeyabana ka (Mwenye kiranga)
Mi maskini jeuri sitegemei madanga (Mwenye kiranga)

Mauza uza we mwana mauzauza
Si wamekushindwa kwenu
Walimwengu tutakufunza

Mauza uza we mwana mauzauza
Si wamekushindwa kwenu
Walimwengu tutakufunza

Unani ni kichwa cha chikichi
Umevaa kinu unatwangia mchi aah

Mwali kigego mwenye nyota ya mitara
Hivi kungwi wako nani wewe? (Atajijua)
Uso mitego imedoda biashara
Hueleweki si kunguru si mwewe

Wadala ubaki dala mwenzio mimi kibunja
Haufai kwa kafara si puzi wewe ni punja
Umejivesha ubezezi kwa mapana na marefu
Uso na kazi si wa ndala wala peku

Ooooh ondoa ndo mlezi wa hana
We ebu ndege zoa zoa'
Mwali pengo binti mwanya
Tuchunge kwa kudonyoa

Oooh leo nikome (Mwenye kiranga)
Hujalijua vizuri litimbwi ni la vanga (Mwenye kiranga)
Oooh leo boda umeyabana ka (Mwenye kiranga)
Mi maskini jeuri sitegemei madanga (Mwenye kiranga)

Oooh leo nikome (Mwenye kiranga)
Hujalijua vizuri litimbwi ni la vanga (Mwenye kiranga)
Oooh leo boda umeyabana ka (Mwenye kiranga)
Mi maskini jeuri sitegemei madanga (Mwenye kiranga)

Mauza uza we mwana mauzauza
Si wamekushindwa kwenu
Walimwengu tutakufunza

Mauza uza we mwana mauzauza
Si wamekushindwa kwenu
Walimwengu tutakufunza

(Hahaa kuvaa dera si kazi, kazi kulikamatia eeh)

Utayaweza yangu, yako yanakushinda
Utayaweza yangu, yako yanakushinda(Ooooh tikisa ndole)
Utayaweza yangu, yako yanakushinda(Uso kasi mwana wako)
Utayaweza yangu, yako yanakushinda (Oooh...nadilidadi)

Utayaweza yangu, yako yanakushinda 
(Usonoga kwa chumvi wala magadi)
Utayaweza yangu, yako yanakushinda

Watch Video

About Mauzauza

Album : I am Zuchu EP / Mauzauza (EP)
Release Year : 2020
Copyright : (c) 2020 Wasafi Records.
Added By : Huntyr Kelx
Published : Apr 13 , 2020

More lyrics from I Am Zuchu album

More ZUCHU Lyrics

ZUCHU
ZUCHU
ZUCHU

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl