YOUNG KILLER Sinaga Swagger 4 cover image

Sinaga Swagger 4 Lyrics

Sinaga Swagger 4 Lyrics by YOUNG KILLER


[Intro]
Ni kijana aliyepitia makubwa 
Kwenye safari yake ya mafanikio
Ukizungumzia kukesha usiku 
Kutafuta nafasi za  kuperform
(Bro naomba nichane)

Kukataliwa kwenye jamii
Na watu kumwaminisha kuwa hawezi
Na mbaya zaidi hata familia yake
Walikosa imani juu ya kipaji chake

Na kumuusia asome sababu muda mwingi
Alikuwa akionekana akideal na muzuki
Lakini, siku zote Mungu huwa 
Hamtupi mja wake

Baada tu ya kupata nafasi 
Aliitumia ipasavyo 
And now  it's proof to the world
The real meaning of a Young KILLER

[Verse]
Zinazofanya tugombane ni doh
Mpaka tunachukiana na mwisho tutoane roho
Kujifanya magangster kumbe ndani bishoo
Kupandishana mapresha kuua shingo na roho

Nilifika mchanaji mmoja matata
Hapo through-back ya Tabata
Pindi ya mambo ya Basata
Nilijua mlipata hii mkasema(Aaah sema weee)
Kwenye frame ni mdogo wasitune paja
Wambie madogo waache nyodo
Bro wao wasipompenda kaja

Haina haja kuleta jam jam zama hizi
Kumwambia nyani asali ni tamu kuliko ndizi
Kumgombanisha mvivu na usingizi
Yaani kucheka kwa furaha 
Na mhalifu wako wakati wa fumanizi
That's easy brother mambo ya trending
Sorry for long time now nothing change

Leo shetani kachelewa kuamka
Kwa hiyo mapema yale mambo makuu mawili
Na mkuu ndio kasema 
Sio kesi kurefresh na kuinvest
Inadepend na pocket yako 
Ila hatukopeshi na hatukeshi
Kuna muda wa mapenzi na business
Na ucheshi na kudance na mabeste na mafifa
Na mepesi eyoo majani yaani

Niwe majani mpande mawe
Niache mali shambani
Nikatafute kwenye changalawe
Kazeni kumtoa Messi LaLiga 
Aje kucheza aje kucheza kikapu

Tuweni sharp rasta supu inanywewa ikiwa moto
Mimi ni kikipaka hapa hata ukikaa ufukweni joto
Nilikuwa msoto mwanzo nakumbuka mama alilia sana
Akanambia vumilia chana

Elimu dunia sio elimu ya kupuuza
Sio kila baya baya mengine mabaya yanafunza
Mwanafunzi ukifanya kitu ambacho 
Hakija nifurahisha kwenye macho 
Nakupiga hata Kawa mwalimu mkuu mama ako

Sikosi kugusa legeza chujio chicha zipite
Alafu nipe heshima sio mpaka nife mnizike
Na mliziba matundu yote nisipite
Msijali nitaombea Mungu hiyo dhambi asiandike

Wengi wanafurahi ninapo anguka 
Hawapendi nikamate line
Acheni wanikazie ili -- wengine washine
Ila mnanicompare mi na watoto wa kuja

Ni kutoa ndogo wakati una bata ni likubwa
Yaani ishindane na muda hata uwe nunda hushindi
Utavuga tu kwa wahuni alafu kwa mchumba haudindi
Na siku ntayo shindwa na mapimbi

Haki natembea nakunya toka 
Mwanza kuja Dar mpaka Lindi
Nasishindwi kubeba jamii kujiamini
Napita zzzz zaidi ya dawa ya ukimwi

Mimi mtu mpole wewe aka mshamba kabambe
So ukijifunika blanketi alafu ukajamba jipambe
Eti ujimiz na watoto wa fisi alafu upitwe na ibilisi
Yaani uende urudi unamtaka Shishi
Ivi unahisi kirahisi uchebe utakuchekea
Si sawa ung'oe jino alafu utembee unachechemea

You will cry when am dying nimjue friend
Kama kusubui hakupendi, all eyes on me 
If you love me, love me and show me 
Life is a lesson na sina test for me

Kama hamjui mnapokwenda kwa hiyo
Sehemu mliokuepo mtahisi mmefika
Ni funzo hii sauti inaposikika
Japo inaua na kuzika 
Tafuteni mikwanja mtadhalilika
Asanteni na poleni kwa pilika(Hiii hahahahha)

Right now you already know who I am
Big shout out to all haters and money makers
Lengo letu si kuishi milele 
Ni kufanya vitu vitavyoishi milele
Mambo mazuri yako mbele kwa mbele
Usikate tamaa msela ongeza misele

I told you, not funny
Hey leaders this time to wake up
Cause Young Killer Msodoki hahahaha
Ujue mimi sinaga swagga kabisa yaani
Eeh natoka Mwanza, Mwanza eeh Mwanza 
Kwani vipi?

Watch Video

About Sinaga Swagger 4

Album : Sinaga Swagger 4 (Single)
Release Year : 2020
Copyright : (c) 2020
Added By : Huntyr Kelx
Published : Mar 12 , 2020

More YOUNG KILLER Lyrics

YOUNG KILLER
YOUNG KILLER
YOUNG KILLER
YOUNG KILLER

Comments ( 1 )

.
5963 2020-03-23 06:22:03

Nakubal sana



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl