MACVOICE Bora Peke Yangu cover image

Bora Peke Yangu Lyrics

Bora Peke Yangu Lyrics by MACVOICE


(Eyoo Trone)
Heshima na upole wako
Ndivo vikanivuta kwako oh oh
Tabia na mwenendo wako oh
Vikanifanya nikupende eh eh

Kumbe mapenzi ni nyakati yanachanganya
Yakipoteza ramani wewe
Kitabu cha upendo wa dhati umechanachana
Haupo kama zamani wewe

Ngoma ikivuma mwisho wake hupasuka
Yote ya nini tuje kushikiana chupa
Wewe ukipanda kila muda mi nashuka
Oh ooh oh, oh oh oh

Message za watu wako na simu zako
Naona ila namezea tu
Najua machafu yako mabaya yako
Yanachoma mi napotea tu

Kugombana mi siwezi
Nikwambie yote sababu ya mapenzi
Tena narudisha jezi nitulie
Ligi ya mapenzi siwezi

Kwako wewe, bora peke yangu
Nibaki peke yangu
Bora peke yangu
Niishi maisha yangu

Bora peke yangu
Nibaki peke yangu
Bora peke yangu
Niishi maisha yangu

Uliweka pamba masikioni
Husikii huoni ninavyoumia moyoni
Purukushani asubuhi jioni
Matusi mdomoni hata aibu huoni

Ukadanganya unaenda sokoni
Kumbe yuko mgongoni kitandani ukingoni
Una wapenzi wengine kinondoni
Hadi Kigamboni na Kariakor shimoni

Ah wee, kumbe ni mnyama uloficha makucha
Hata sura yako inakusuta
Nyama ndani ngano nnje kama sambusa
Barafu wa moyo umeyeyuka
(Oh wo wo wo wo, oh wo wo wo wo)

Hukunipenda, pengine nilikulazimisha
Sawa nakwenda, japo sina wa kuninyamazisha
Huna makosa najilaumu nini?
Nilikupenda kwa nini?

Ona kugombana mi siwezi
Nikwambie eti sababu ya mapenzi
Tena narudisha jezi nitulie
Ligi ya mapenzi siwezi

Kwako wewe, bora peke yangu
Nibaki peke yangu
Bora peke yangu
Niishi maisha yangu

Bora peke yangu
Nibaki peke yangu
Bora peke yangu
Niishi maisha yangu

(Nusder)

Watch Video

About Bora Peke Yangu

Album : My Voice (EP)
Release Year : 2021
Copyright : (c) 2021 Next Level Music
Added By : Huntyr Kelx
Published : Sep 25 , 2021

More lyrics from My Voice album

More MACVOICE Lyrics

MACVOICE
MACVOICE
MACVOICE

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl