ZABRON SINGERS Nitasubiri cover image

Nitasubiri Lyrics

Nitasubiri Lyrics by ZABRON SINGERS


Ya nini Mungu kujificha wakati wa shida?
Wakati mwingine kama kweli huoni
Wajua yote yalonikuta hasimliki
Nimelia na kujinyamazisha pekee yangu

Moyoni nikataabika, furaha ikaenda
Sikumwona wa kumwelezea shida
Rafiki pekee namwamini, ni Yesu mfariji
Ndio maana sijamwambia mtu shida zangu

Nitasubiri na kusubiri sitachoka
Nimeshamezana na wewe kwa maombi
Usipojibu, au ujibu nitaelewa
Nashukuru, hata kwa majaribu
Mungu unasababu mimi kuishi maisha kama haya

Nitasubiri na kusubiri sitachoka
Nimeshamezana na wewe kwa maombi
Usipojibu, au ujibu nitaelewa
Nashukuru, hata kwa majaribu
Mungu unasababu mimi kuishi maisha kama haya

Kwa nini sasa umesimama mbali nami Bwana?
Muda mwingi mi najihisi mi ni mpweke
Jidhihirishe mi nikuone, nakuhitaji Bwana
Nibariki sasa ukijibu maombi, yangu

Najua mengi nimekuudhi, nimetenda dhambi
Ndio maana ukasimama mbali nami
Nisamehe yote yote bure, kwa damu ya Yesu
Nifanye mi niwe mtoto wako siku, zote

Nitasubiri na kusubiri sitachoka
Nimeshamezana na wewe kwa maombi
Usipojibu, au ujibu nitaelewa
Nashukuru, hata kwa majaribu
Mungu unasababu mimi kuishi maisha kama haya

Nitasubiri na kusubiri sitachoka
Nimeshamezana na wewe kwa maombi
Usipojibu, au ujibu nitaelewa
Nashukuru, hata kwa majaribu
Mungu unasababu mimi kuishi maisha kama haya

Watch Video

About Nitasubiri

Album : Mkono wa Bwana (EP)
Release Year : 2019
Copyright : (c) 2021
Added By : Huntyr Kelx
Published : Jan 17 , 2021

More lyrics from Mkono wa Bwana (EP) album

More ZABRON SINGERS Lyrics

ZABRON SINGERS
ZABRON SINGERS
ZABRON SINGERS
ZABRON SINGERS

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl