...

Jivunie Chako Lyrics by ZABRON SINGERS


Ndoa ni kkwanza kuelewana (sio fujo, mateke na ngumi)

Ndoa ni kkwanza kuelewana (sio uwanja wa mapambano)

Umtunze mkeo, umpende mmeo

Huyo ndiye wako, kipenzi cha moyo wako

Umtunze mkeo, umpende mmeo

Jivunie chako, fuhara ya moyo wako

Nawahasa msigoùbane tena

Na ndoa yenu msilie tena, uliyempata leo ndiye kipenzi chako

Siunajua mmekubaliana

Kweli ni kwamba nyie mnapendana

Ndio maana tumekuja leo

Tumalize jambo lenu

Hivi unajua ilikuwaje

Mpaka huyo eva apatikane

Huyo eva alitoka kwenye ubavu

Ubavu wa mwanaume

Adamu kasema sasa huyu mifupa katika mifupa yangu

Na nyama katika nyama yangu

Ataitwa mwanamke

Kwa hiyo sasa huyo mwanaume, atamuacha baba yake

Atamuacha baba yake na mama yake tena

Aambatane na mkewe, wakaishi kwa fuhara

Watakuwa mwili mmoja wataishi pamoja

Hivi unajua ilikuwaje huyu bi harusi apatikane

Bwana harusi hatika amepambana ampate kipenzi chake

Twawaombea mkafurahi vicheko utani na raha nyingi

Watu wote leo tuko hapa tumalize jambo lenu

Ndoa ni kwanza kuelewana (sio fujo, mateke na ngumi)

Ndoa ni kkwanza kuelewana (sio uwanja wa mapambano)

Umtunze mkeo, umpende mmeo

Huyo ndiye wako, kipenzi cha moyo wako

Umtunze mkeo, umpende mmeo

Jivunie chako, fuhara ya moyo wako

Watu wamekuja kuwapa mji ndugu na rafiki

Wote wamefurahi kuwa hapa kwa ajili yenu

Basi sasa msipigane mpendane mchukuliane mbebane

Mvumiliane muwe wakufichiana siri

Ugomvi na hasira hasira msifanye mueleweshane kwa upole

Majibu mazuri upalilia upendo

Na kwa sasa sisi tumeridhika taratibu zote mmezifata

Kama vile bwana mungu aliagiza, mfunge ndoa takatifu

Kikubwa sasa twawaombea mungu awape maisha marefu

Yenye baraka furaha pia upendo katika nyumba yenu

Basi sasa msipigane mpendane, mchukuliane mbebane

Mvumiliane muwe wakufichiana siri

Ugomvi na hasira hasira msifanye mueleweshane kwa upole

Majibu mazuri upalilia upendo

Usimpige mkeo utakuwa wajipiga mwenyewe

Maana sasa nyinyi ni mwili mmoja

Utajiumiza mwenyewe asipoumia mwili atakua ameumia moyo

Nawe pia utajiumiza moyo, furaha ukosekana

Ndoa ni kwanza kuelewana (sio fujo, mateke na ngumi)

Ndoa ni kkwanza kuelewana (sio uwanja wa mapambano)

Umtunze mkeo, umpende mmeo

Huyo ndiye wako, kipenzi cha moyo wako

Umtunze mkeo, umpende mmeo

Jivunie chako, fuhara ya moyo wako

Watch Video

About Jivunie Chako

Album : (Single)
Release Year : 2025
Copyright :
Added By : Farida
Published : Mar 28 , 2025

More ZABRON SINGERS Lyrics

ZABRON SINGERS
ZABRON SINGERS
ZABRON SINGERS
ZABRON SINGERS

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2025, We Tell Africa Group Sarl