MARTHA MWAIPAJA Hatufanani cover image

Hatufanani Lyrics

Hatufanani Lyrics by MARTHA MWAIPAJA


Oooh, ooh ooh...
Hatufanani, hatufanani
Kuna neema inanibeba mimi, hatufanani
Hatufanani, hatutafanana
Kila mtu na neema yake, hatufanani

Hatufanani, hatutafanana
Kila mtu na neema yake, hatufanani
Hatulingani, hatutalingana
Kila mtu na neema yake, rafiki, hatufanani

Kwa Neema ya Kristo tunaendelea mbali

Nimetoka mbali mimi hakuna aliyejua niliyopitia
Iligharimu Mungu aje anisaidie, mimi kuwa salama
Iligharimu Mungu ashuke aniambie neema iko na wewe
Nililalamika kwa Mungu kwa nini magumu yanipate mimi

Nikasema nimekosa mimi sana, mbona kila siku nalia mwenyewe tu
Nikasema kwa nini na yule aliye kama mimi
Nikalalamika nikasema kila siku ni mimi ninayeteseka
Iligharimu Mungu aje kwangu aniambie Mwanangu ipo neema
Kwa upole akaniambia wanadamu hamtafanana
Nikasikia natiwa nguvu kwamba wote hatutafanana

Hatufanani, hatutafanana
Kila mtu na neema yake, hatufanani
Hatulingani, hatutalingana
Kila mtu na neema yake hatufanani

Hatufanani, hatutafanana
Kuna neema inanibeba mimi, hatufanani
Hatulingani, hatutalingana
Kila mtu na neema yake wewe, hatufanani

Hatutafanana, mimi na wewe
Ni neema tu inatusaidia
Mungu peke yake ametusaidia

Ninashukuru kwa Mungu wangu hatazami kama mwanadamu
Ninashukuru kwa Yesu wangu hachagui nani amsaidie
Mnionavyo ni Mungu tu, sijatoka hapa rafiki huh
Nimetembea kutoka mbali, usinikasirikie mwenzio
Usitake nianguke chini, kuna neema inanisaidia hatufanani
Usichimbe shimo nitumbukie, kuna nguvu imenivusha kule hatufanani
Ungepewa neema ujue nilikotoka, ungesema kweli hatutofanani

Hatufanani rafiki, neema yangu na yako si sawa
Usinipangie mabaya kwa siri, kuna neema imenisaidia
Mimi nawe hatufanani neema yangu tu imenisaidia
Hatufanani rafiki tusichukiane, kila mtu na neema yake tu
Hatufanani

Hatufanani, hatutafanana
Kila mtu na neema yake, hatufanani
Hatulingani, hatutalingana
Kila mtu na neema yake hatufanani

Hatufanani, hatutafanana
Kuna neema inanibeba mimi, hatufanani
Hatulingani, hatutalingana
Kila mtu na neema yake wewe, hatufanani

Kwa mkono wa Mungu tunaendelea
Kamwe hatutafanana haa
Asante kwa Mungu wangu
Asante kwa Yesu wangu
Anayetusaidia Halleluyah

Watch Video

About Hatufanani

Album : Hatufanani (Single)
Release Year : 2021
Copyright : (c) 2021
Added By : Huntyr Kelx
Published : Aug 12 , 2021

More MARTHA MWAIPAJA Lyrics

MARTHA MWAIPAJA
MARTHA MWAIPAJA
MARTHA MWAIPAJA
MARTHA MWAIPAJA

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl