ASLAY Mchepuko cover image

Mchepuko Lyrics

Mchepuko Lyrics by ASLAY


Unapoelekea mchepuko wangu 
Unanichosha mwenzenu
Wa kumliza liza mke wangu
Jamani unanichosha mwenzenu

Hata kama niko nawe kimwana
Utulivu unatakiwa
Mimi bado nina mwenyewe kimwana
Utulivu unatakiwa

Unamrusha roho kwanini?
Unamtambia amekosa nini
Unaharibu hivyo, nyumbani
Ananililia kila siku mimi

Na unajua kumwacha siwezi 
Kanizalia watoto mwenzako
Nguvu za kushaua unaharibu kichizi
Unanipa changamoto mwenzako aah

Unamvalia mini akivaa dera
Unachenjigi mawig 
Hata kama sijakupa hela

Wewe una iPhone mwenzako ana Motorolla
Unashindana na Gigi 
Kwenye mabendi kutunza hela 
Vibaya hivyo

Mchepuko, mchepuko
Unaumiza mke wangu
Mchepuko, mchepuko
Unaumiza mke wangu

Nakupa mapesa unaninita sponsor
Unaniongopea unanikosea
Tatizo ni hicho kishepu na sura chako 
Ndo kinanipa mawazo mwenzako

Nashindwa kukuacha mwenzako
Oooh nitafilisika juu yako mchepuko

Unamvalia mini akivaa dera
Unachenjigi mawig 
Hata kama sijakupa hela

Wewe una iPhone mwenzako ana Motorolla
Unashindana na Gigi 
Kwenye mabendi kutunza hela 
Vibaya hivyo

Mchepuko, mchepuko
Unaumiza mke wangu
Mchepuko, mchepuko
Unaumiza mke wangu

Anakujua, anakujua
Unavyomjua mama watoto 
Atakufanyizia siku moja

Anakujua, anakujua
Unavyomjua mama watoto 
Atakufanyizia 

Watch Video

About Mchepuko

Album : Mchepuko
Release Year : 2020
Copyright : (c) 2020
Added By : Huntyr Kelx
Published : Apr 18 , 2020

More ASLAY Lyrics

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl