Mwana Lyrics by JOEL LWAGA


Nilifikiri moyoni mwangu
Nikamwambia Baba 
Nipe sehemu ya mali yangu

Nikaondoka nyumbani kwetu
Nikaenda mbali
Nikatumia mali yote

Nikacheza na muda
Nikaruhusu mali initawale
Eeh eeh

Maisha yakawa magumu 
Nikafikiri moyoni mwangu
Nitaenda wapi? 

Eeh Nyumbani
Nimeshaondoka aah
Nitafanya nini mimi?
Mwana mpotevu

Aah.. aah

Nilipozingatia
Moyoni mwangu mimi
Nikaona bora nirudi kwa baba

Yanini kuendelea 
Kula na nguruwe hapa
Wakati watumishi wa baba 
Nyumbani wanakula na kusaza

Oooh nikaona bora nirudi
Kwa baba nitamwambia nimekosa
Ju ya mbingu na mbele yako
Sistahili tena kuitwa mwanao
(Oooh oooh)

Lakini baba aliponiona
Kutoka mbali akanikimbilia
Akanivika mavazi mazuri
Na pete kidoleni mwangu 
(Aah aah)

Akanikumbatia 
Na kunibusu shingoni
Akaamuru sherehe ifanyike

Maana mwanae aliyekufa
Sasa anaishi tena
Mwanae aliyepotea
Amerudi

Akasema sitakufanya
Kuwa mmoja wa wajakazi wangu
Wewe ni mwanangu aah
Wewe ni mwanangu (Aah mmmh..)

Watch Video

About Mwana

Album : Thamani EP (EP)
Release Year : 2020
Copyright : (c) 2020
Added By : Huntyr Kelx
Published : Aug 01 , 2020

More lyrics from Thamani (EP) album

More JOEL LWAGA Lyrics

JOEL LWAGA
JOEL LWAGA
JOEL LWAGA

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl