Paradiso Lyrics by STAMINA


Tuonane paradiso
Tuonane paradiso
Tuonane oh paradiso
Tuonane paradiso

Najua wengi mnaumia mtu akiwa hoi mahututi
Kila nafsi ni ulimi lazima itaonja mauti
Wengi wenu dah mnalia kinafiki
Mnasahau kwamba mshahara wa dhambi 
Haulipagwi benki ndugu

Najua mnakuwa wengi msibani
Ila kipindi cha wacha ajabu mbona hatuonani
Moyo wangu unaniuma sana ila wacha nibaki bubu
Bora kidonda rafiki kuliko kidonda ndugu
Ila presenter anaongea kama anajua 
Wakati nishamuomba interview mara kibao na akazingua
Na ndo maana sikutoaga rushwa kwa dj
Nilijua tu nikifa mtapiga bure bila pay
Nishapeleka nyota yangu kwa waganga mara ngapi?
Ushanisimanga kwa maneno hadi ukachoka kiko wapi
Binadamu aliyekamilika haya nionyeshe yuko wapi
Kama malipo duniani sema nikulipe shingapi

Mshaniteka, mkanitesa mkanifanya mnachotaka
Mshanifunga hadi jela bila hatia kisa mamlaka
Usinyanyase haki ya nani nakwambia
Na wote mnaotembea leo hii ni marehemu watarajiwa

Wanaolia hawahesabiki
Ijapo hawakunipenda zamani
Wanafiki leo marafiki
Hawana hata haya usoni
Wanasubiri mpaka nife
Ndo sifa zangu zije ziskike

Mmeniwekea mashada ambayo siwezi hata kuyanusa
Jeneza la bei ghali ambalo siwezi hata kuligusa
Mmepika hadi waba ambao siwezi hata kuonja
Wakati hamkuleta matunda kipindi nilipokuwa mgonjwa

Rafiki wa kweli ni yupi? 
Anayekunyenyua wakati unaanguka
Hawa anahakikisha anakuangusha unapoinuka
Maana rafiki wa karibu waliniona kama mzigo
Ungenipa moyo inatosha si lazima wanipe figo

Wasanii wezangu jau, nadhani mshasahau
Nishatuma sana macover hamkuposti
Au mlitaka dau, leo nimekufa ndo mnaposti 
Vipi mnangoja nije nikomenti au

Boss nilifanya kazi kubwa na hukunipa mshahara wangu
Na bado ukaona haitoshi ukatembea na mke wangu
Ukaleta simanzi mpaka kwa watoto wangu
Nashangaa leo unamwanga machozi kwenye msiba wangu

Nimeona rambirambi ya rais, hivi kaileta nani
Najua yuko busy kuwashinda kambi ya upinzani
Ningekuwa hai ningemfanyia hata kampeni
Kazi ya Mungu haina makosa, wote tuseme AMEN

Wanaolia hawahesabiki
Ijapo hawakunipenda zamani
Wanafiki leo marafiki
Hawana hata haya usoni
Wanasubiri mpaka nife
Ndo sifa zangu zije ziskike

Bora uzikwe ukiwa hai
Kuliko kuishi kwenye dunia
Wanatamani ukatishwe uhai
Japo usoni wanakuchekea 

Binadamu, hawa binadamu
Binadamu wouwooo...

Wanaolia hawahesabiki
Ijapo hawakunipenda zamani
Wanafiki leo marafiki
Hawana hata haya usoni
Wanasubiri mpaka nife
Ndo sifa zangu zije ziskike

Watch Video

About Paradiso

Album : Paradiso (Album)
Release Year : 2021
Copyright : (c) 2021
Added By : Huntyr Kelx
Published : Dec 08 , 2021

More STAMINA Lyrics

STAMINA
STAMINA
STAMINA
STAMINA

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl