Baba Lyrics by STAMINA


Kwanza naomba ukae chini alafu uvute pumzi
Nina vitu vya kuongea ambavyo najua vitakuudhi
Hivi unajua nimekuvumilia sana
Angekuwa mtoto mwingine tayari ungeshampa laana

Najiuliza sijui nikuseme na kipi baba
Najiuliza sijui nianze na lipi labda
Mama anasema mwanzo mimba ulikataa
Kwanini sasa hukutoa ukaruhusu mpaka akazaa?

Alafu hivi hauzijui kinga
Haukujua pekupeku kama italeta mimba
Uchi wako wa kijinga ndo saa hivi unanitesa
Usingemrubuni mama labda angemuoa bakresa

Dah, unanipa kiwewe
Au manesi walichanganya babangu haukuwa ni wewe
Kama unataka kunipiga we yote sawa
Au nikuchumie fimbo unichape kisawa sawa

Hata kama ni mzazi
Saa zingine nawaza nikuchukie
Sema tu we ni mzazi
Acha ukweli wako nikwambie

Daddy iii, naongea na wewe eh
Daddy iii, naongea na wewe
Naongea na wewe

Ile hela ya kuhonga ungetoa ka sadaka
Mungu angekubariki ungenizaa kama baraka
Ukajichanganya kaisari ukampa hisiaka
Alafu mbele ya Yesu Petro ukampa mamlaka

Mbona Mzee Mushi namuona na hela
Mzee Mwakalinga mwenzio ana hela
Mzee Luta Shobwa ndo kabisa na mihela
Wewe ulikuwa wapi mpaka unakufa kabwela

Nikuulize, ukifa nitaridhi nini?
Labda jina la ukoo alafu linisaidie nini?
Utajiri hivi haukuona kwanini
Maana pombe unazokunywa siwezi ridhi hadi maini

Umeshindwa hata kununua kiwanja
Ona mpaka leo tupo nyumba za kupanga
Elimu siku hizi ni bure
Ila cha ajabu umeshindwa kunipeleka shule

Inauma sana ila acha tu nikuulize
Ina maana ujana wako umeshindwa kuwa busy
Nikiendelea kuongea naona kama nitakufuru
Nakuombea kwa Mungu akupe nuru

Hata kama ni mzazi
Saa zingine nawaza nikuchukie
Sema tu we ni mzazi
Acha ukweli wako nikwambie

Daddy iii, naongea na wewe eh
Daddy iii, naongea na wewe
Naongea na wewe

[Professor Jay]
Mwanangu nimekuskia nakuombea kuwa uyaone
Nilijua umekuja kwangu kuniombea ili nipone
Kumbe umekuja na shari kunilaumu na kunihukumu
Inaonyesha ningesinzia ungeninywesha hata sumu

Baada ya ujauzito wako tulipima na mamako
DNA ilionyesha kuwa mimi sio damu yako
Ukiskia ukubwa hujalala basi jua dunia ni dambo
Nikasimama kidete kupigania maisha yako

Tena nilingoja ngoja ukue
Nikajitoa kwa hali na mali ili usijue
Nikafanya mambo mengi hatari ili nikutunze
Wakanisweka jela ili dunia inifunze

Ukuwaji wako sidhani ulilishwa mila
Nilipambana kila kona kuwataftia ngawila
Niliuza mali zangu ilimradi wewe usome
Leo unanipandishia kibase nyambavu tena unikome

Mwone mtoto wa Sobo, mwenzio ni rubani
Mtoto wa Sugu juzi kapata udiwani
Mtoto wa Bwire ndo daktari marekani
Hebu toa bangi zako, aliyekuambia usisome nani?

Hata kama ni mzazi
Saa zingine nawaza nikuchukie
Sema tu we ni mzazi
Acha ukweli wako nikwambie

Daddy iii, naongea na wewe eh
Daddy iii, naongea na wewe
Naongea na wewe

Hata kama ni mzazi
Saa zingine nawaza nikuchukie
Sema tu we ni mzazi
Acha ukweli wako nikwambie

Daddy iii, naongea na wewe eh
Daddy iii, naongea na wewe
Naongea na wewe

Watch Video

About Baba

Album : Baba (Single)
Release Year : 2021
Copyright : (c) 2020
Added By : Huntyr Kelx
Published : Jan 13 , 2021

More STAMINA Lyrics

STAMINA
STAMINA
STAMINA

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl