NIKKI MBISHI Maneno ya Mashabiki cover image

Maneno ya Mashabiki Lyrics

Maneno ya Mashabiki Lyrics by NIKKI MBISHI


Nikki Mbishi ana chuki ana wivu ana gubu
Mziki umemshinda hana kitu anatubu
Anaishi chumba kimoja anajitia kiburi sugu
Fid alisema hana nidhamu mithili ya wile wadudu 
Stress zimemjaa ye ni pombe tu na ndumu

Game imebadilika ye anakomaa tu na ngumu
Tv zimemchoka na redio zimemtosa
Anaposti tu mashairi kweli soko limemnyoosha
Wenzake wanapiga mchele kimya kimya bila kwere

Wana magari tele na majumba kama Mbere
Kazi yake kuponda ponda hana fact wala mantic
Anaota kuna siku ata-sign iwa na Atlantic
Anajidai mjuaji hapendwi hana washikaji

Hana tuzo wala taji nini Benzi ama Bajaji
Kifupi jamaa mzugaji, mamluki msindikizaji
Anakuletea uzushi anadai uhai ni maji

Ni mashabiki, wanavyosema
Mziki umemkimbiza anahema
Hata kiki hapati tena
Pabaya panamwita hataki pema

Ni mashabiki, wanavyosema
Mziki umemkimbiza anahema
Hata kiki hapati tena
Pabaya panamwita hataki pema

Alijifanya anaacha mziki njaa ikazidi akarudi
Anadiss kupata kiki hapo ndipo anapo bugi
Kipaji Mungu kambariki tatizo hafanyi juhudi
Ukimwambia ukweli anakublock hana budi

Anaita wenzio ma-whack 
Redioni hana hata hit song
Nahisi anavuta unga
Maana ana ushikaji na King Kong
Ruki mwenyewe hasikiki si apige ngoma na Ringtone
Abbah na Mr T Touch wanaotawala kingdom
Japo duction inapunguza harakati
Mziki umejaa corruption na yeye rushwa hataki

Wenzake wanaachia ngoma zinatrend kwenye chati
Wengi wanatake over kwake haplay ya manati
Haendi na wakati ana swagga pale kati
Umri umezidi kwenda na ametengwa na kamati

Anaendekeza jenga sijui atajenga wapi
Anashindwa na Dogo Njanja sababu anapenda unafiki

Ni mashabiki, wanavyosema
Mziki umemkimbiza anahema
Hata kiki hapati tena
Pabaya panamwita hataki pema

Ni mashabiki, wanavyosema
Mziki umemkimbiza anahema
Hata kiki hapati tena
Pabaya panamwita hataki pema

Ukiacha sauti ya jogoo
Hana tena album kali
Video zake zote mbovu
Wenzake wanaskika mbali

Mziki umemwacha chali siku hizi anauza mistari
Tangu enzi za JK haalikwi taftari ya ikulu
Itakuwa vipi usawa huu wa Magu? 
Sanaa haimlipi hata aseme aende kwa babu

Anajiona special wakati maajabu hana
Asipofanya commercial atapata taabu sana
Maana kipigo chake ni zaidi ya Mr Nice
Jinsi alivyofulia hapati hata Insta likes

Akitaka tumkubali, ajipange aje tena
La sivyo hasikiki tena hadi Mange akisema
Aache bangi akitema hapo brand ataijenga
Apate manzi kama Nandy amfanye ka Bill Nenga

Nikki mbishi, Nikki mbishi kitu gani
Wenzako wamewasha more fire hamwoni kitu hewani

Ni mashabiki, wanavyosema
Mziki umemkimbiza anahema
Hata kiki hapati tena
Pabaya panamwita hataki pema

Ni mashabiki, wanavyosema
Mziki umemkimbiza anahema
Hata kiki hapati tena
Pabaya panamwita hataki pema

Watch Video

About Maneno ya Mashabiki

Album : Maneno ya Mashabiki (Single)
Release Year : 2020
Copyright : (c) 2020
Added By : Huntyr Kelx
Published : May 09 , 2020

More NIKKI MBISHI Lyrics

NIKKI MBISHI
NIKKI MBISHI
NIKKI MBISHI
NIKKI MBISHI

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl