NAY WA MITEGO Rais wa Kitaa  cover image

Paroles de Rais wa Kitaa

Paroles de Rais wa Kitaa Par NAY WA MITEGO


Niliyesimama mbele yenu sio mbunge ni msanii
Natumia sanaa kuitetea jamii
Naongea nikiwa Bongo sitakimbia kama Roma
Mkiniteka mkinifunga bado dunia itasonga

Nani kamwambia mheshimiwa eti tumekubali tozo
Hapana sio Tanzania labda Zambia au Congo
Makato ni makubwa wananchi wanaumia
Hivi ni kwamba hamskii au ndo mnapuuzia?

Mishahara ya wabunge ni jasho la wananchi
Spika naongea na wewe kwa niaba ya wenye nchi
Kuna wabunge kumi na tisa walishafukuzwa na chama
Chadema ina maana hawana chama

Na bado nao bungeni na wanapokea mshahara
Hivi unatuchukulia aje unatuona bongolala?
Wimbo ulianza taratibu na sasa umepamba moto
Unapendwa na wananchi kwa viongozi kaa la moto

Katiba mpya ni sasa, katiba mpya ni sasa
Wanaoimba ni wananchi pamoja na wanasiasa
Mafuta bei juu, gesi bei juu
Kila kitu bei juu, mtatuua mwaka huu

Sukari imepanda bei
Luku tozo pesa wapi nitakope?
Nani atusemee, semee sisi wanyonge
Wacha niwasemee
Nani atusemee, semee sisi wanyonge
Rais wa Kitaa

Sukari imepanda bei
Luku tozo pesa wapi nitakope?
Shebi huku miriamu wameikataa
Chombo mikokote

Nani atusemee, semee sisi wanyonge
Ni Rais wa Kitaa
Nani atusemee, semee sisi wanyonge
Tusijiite wanyonge hapana nakataa

Mi ni mmoja kati waliosema unaupiga mwingi
Nahisi una makocha wengi watakukosesha vingi
Nilikwambia hawakupendi wameshakuingiza kingi
Wanakitaka hicho kiti wana tamaa hao madingi

Hey wapi na wapi? Nchi ya wapi?
Mpangaji analipa kodi na tozo ya jengo
Huu ni wizi na mnaiba bila kutumia akili
Hivi nani anawashauri, mnajichimbia kaburi

Uchumi hukua kwenyu kwa wananchi sufuri
Siku hazigandi ni swala tu la muda
Acha iendelee kunyesha tuone panapo vuja

Oyaa wanangu wee, Corona kweli ipo
Nawa mikono vaa barakoa kwenye mkusanyiko
Nchi na mambo hii yataka moyo kuwa mpinzani
Yaani unabambikiwa kesi na unasota gerezani

Mnajenga mimba za chuku hamjifunzi kwa majirani
Mbunge lenyewe chama kimoja si mfute tu upinzani
Mbaki wenyewe tusitafute mchawi nani?

Sukari imepanda bei
Luku tozo pesa wapi nitakope?
Nani atusemee, semee sisi wanyonge
Wacha niwasemee
Nani atusemee, semee sisi wanyonge
Rais wa Kitaa

Sukari imepanda bei
Luku tozo pesa wapi nitakope?
Shebi huku miriamu wameikataa
Chombo mikokote

Nani atusemee, semee sisi wanyonge
Nani atusemee, semee sisi wanyonge

Hii ni tozo babu kubwa, babu kubwa
Au sio wanangu sema babu kubwa
'Tozo babu kubwa'

Hii ni tozo babu kubwa, babu kubwa
Au sio wanangu sema babu kubwa
'Tozo babu kubwa'

Ecouter

A Propos de "Rais wa Kitaa "

Album : Rais wa Kitaa (Single)
Année de Sortie : 2021
Copyright : (c) 2021
Ajouté par : Huntyr Kelx
Published : Sep 08 , 2021

Plus de Lyrics de NAY WA MITEGO

NAY WA MITEGO
NAY WA MITEGO
NAY WA MITEGO
NAY WA MITEGO

Commentaires ( 0 )

Aucun commentaire pour l'instant



A propos de AfrikaLyrics

Afrika Lyrics est la plus large collection de paroles de chansons et de traductions d’Afrique. Afrika Lyrics fournit les paroles des musiques de plus de 30 pays africains et des traductions de lyrics de plus de 10 langues africaines en français et en anglais.

Suivre Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl