
Paroles de Salimia Watu
Paroles de Salimia Watu Par JAPHET ZABRON
Si kuna Mungu, Mungu wa watu
Ndiye hutuweka pamoja
Huyu ni ndugu, yule rafiki
Wote ni kitu kimoja
Uwe m Israeli, uwe kabila la Yudah
Muumba wetu mmoja
Si tuliumbwa na Mungu, kuishi kwetu ni Mungu
Na uzima huu ni Mungu
Waishi vipi na watu wako wa mtaani
Hapa duniani
Utu kwa watu ndani yake twaona upendo
Uwapo hai duniani
Salimia watu pesa huisha
Salimia watu, utu ni utu, ongea na watu
Ndio watakuzika kesho
Salimia watu, utu ni utu, waheshimu watu
Pesa huisha
Salimia watu, utu ni utu, ongea na watu
Ndio watakuzika kesho
Salimia watu, utu ni utu, waheshimu watu
Hakuna jambo lisilo mwisho
Hata bado tujivune
Chini uhai, vitu na mali
Hivi vyote ni vya Mungu
Dunia hii tunapita na njia yetu ni moja
Kuna kifo na uzima
Je unatenda ya Mungu, unatimiza ya Mungu
Wamtegemea Mungu
Kwa wema wenu, kwa watu twaona upendo
Upendo wa Mungu
Anatupenda hutuwazia mema kila siku
Tuwapo hai duniani, waheshimu watu
Pesa huisha
Salimia watu, utu ni utu, ongea na watu
Ndio watakuzika kesho
Salimia watu, utu ni utu, waheshimu watu
Pesa huisha
Salimia watu, utu ni utu, ongea na watu
Ndio watakuzika kesho
Salimia watu, utu ni utu, waheshimu watu
Salimia watu, ongea na watu
Salimia watu, waheshimu watu
Salimia watu, ongea na watu
Salimia watu, waheshimu watu
(Ishi na watu wapende watu)
Ecouter
A Propos de "Salimia Watu"
Plus de Lyrics de JAPHET ZABRON
Commentaires ( 0 )
Aucun commentaire pour l'instant
Vous aimeriez sûrement
Essayez l'application Mobile
A propos de AfrikaLyrics
Suivre Afrika Lyrics
© 2025, We Tell Africa Group Sarl