ROMA Anaitwa Roma cover image

Anaitwa Roma Lyrics

Anaitwa Roma Lyrics by ROMA


Anaitwa Roma hakuna wa kumstopisha Roma Roma
Nani wa kunyamazisha Roma Roma
Kazi kuongea ongea kesho yake on air
Kesho kutwa wamepotea 

Anaitwa Roma hakuna wa kumstopisha
Nani wa kunyamazisha Roma Roma
Kazi kuongea ongea kesho yake on air
Kesho kutwa wamepotea 

Wanauliza siku hizi Roma huimbi za kiharakati
Huku wakisema ununio ndo kumbukumbu iliyo baki
Ahh sasa hamtaki mbona hamkumsapoti Mange
Nyinyi mtakuwa wanafki yaani sijui mlikwama wapi

Walivunja dole la mwisho wakaliacha dole la kati(Mmh)
Eeeh hii si ni nchi ya demokrasi mkimind basi mnajua
Sa mbona kamati(Mmmm) Tuiache hayo

Vipi korosho za Mtwara 
Maana wapiga kura wengi wakulima wafanya biashara
Kumnyima mpinzani ajenda, tendetu yaliyo mema
Sio kumpelekea defender mtaani tutie vilema

Chozi ya waTanganyika hayatawaacha salama
Na damu zilizo mwagika milele zitawaandama
Serikali imewapa nafasi wanawake pongezi ifike
Najiona mwenye bahati nikimtazama mwanangu wa kike

Akikuwa akiuliza wale waloniteka nani aliwatuma
Mjibuni mmemzaa mpare ila asiwachukie wasukuma
Najua atanuna najua ya nyuma yatamtia huruma
Asilipe kisasi ashtaki kwa Mungu aipate suna

Na nikiitwa kwa Mungu Baba nikafa 
Sijamuona mtoto, mmpe shada la msalaba 
Aliweke upande wangu wa kushoto 
Na mtapo imaliza ibada iwe ni padi ya paroko
Nguo zangu azipige mnada mmpe albino ama uroko

Mi ni soja niko vitani 
Nikipona unikiss silaha nawaachia maishani
Ibebeni mkomboe taifa maana nchi yenu itaangamia
Viongozi hawana maarifa na hawataki wakosolewe
Wanafanya kazi kwa sifa 

Anaitwa Roma hakuna wa kumstopisha Roma Roma
Nani wa kunyamazisha Roma Roma
Kazi kuongea ongea kesho yake on air
Kesho kutwa wamepotea 

Anaitwa Roma hakuna wa kumstopisha
Nani wa kunyamazisha Roma Roma
Kazi kuongea ongea kesho yake on air
Kesho kutwa wamepotea 

Yuda usimharibie Dani ili ufurahishe mtukufu 
Sisi wote wanao kwanini unapenda sana Yusufu?
Yakobo, baba pesa madaraka umaarufu
Wanaomwapata vijana wanakosa hekima na utu 

Wapunguzie vifungo wafungwa wasio na hatia
Wengine walifuata mkungo kiukweli hawakuwa na nia
Naskia jimbo la Ubungo kuna mtu amelipania 
We umezitungo ni zaidi ya waraka wa Waibrania

Chama kilisha watimua na siasa mlowanunua
Mnapiga bomu mortuary mnajisifu mmeua
Tuliombee taifa tuombee viongozi wetu
Nchi ina miiba so tuwavishe viatu walioko peku

Tusilete uchama kwenye issue za kitaifa
Uongozi ni kuacha alama chanya na kuajibika
Kutekana kuuana sio sifa ya MTanganyika
Ubora ndama ndio unalipa zizi la ng'ombe uhakika

Hongera baba kwa ukusanyaji wa mapato kedekede
Ya kodi na flyover ndio hizo kanyaga twende
Kwetu huduma ya afya ni bora kuliko ndege
Atafanya yote tumuombee na tuimbe Yesu nibebe

Watu wametumbuliwa mwezi mmoja kabla ya kustaafu
Walimu wamesahauliwa mapato yao halafu
Mapolisi mishahara yao bado twapiga tafu
Hospitali boresha tupunguze idadi ya wafu

Anaitwa Roma hakuna wa kumstopisha Roma Roma
Nani wa kunyamazisha Roma Roma
Kazi kuongea ongea kesho yake on air
Kesho kutwa wamepotea 

Anaitwa Roma hakuna wa kumstopisha
Nani wa kunyamazisha Roma Roma
Kazi kuongea ongea kesho yake on air
Kesho kutwa wamepotea 

Sijawai kuona mpga kinanda wa kanisa akitoa sadaka
Cameraman akianguka ndani ya misa kwa pepo kaka 
Na sadaka halali ni ile utaitoa kwa uchungu
Tafta pesa wee siku hizi hulijali sio ukubwa rungu 

Na nyota mshale we bishoo segera 
Ukuki na kulenga tokea hale
Nenda kalete mamluki karoge mambo iko huku
Roma anaiteka show, kafara unamchinjia kuku?

Mi namchinja naichinja kondoo 
Andaa show alafu mmlete mkali wenu tafta venue 
Baada ya dakika mbili mpige mziki ya maiti yenu
Eti unarap? Huwa unarap wewe? Unarap nini?
Ni wanakubeba na hautaamini usiku wakikupiga chini

Sa we kamatia chini mi nakamatia ndinga
Na ukikamatia mpini si utakamatia mimba 
Alafu kizazi nakwacha unang'aza sharubu
Kula nganzi mi kisirani nina gubu

Na elfu mbili na ishirini si tumwombe Mungu
Wewe na mimi na wote wasaka tonge watao rudi vitini
Watuepushe na hiki kikombe mwaskizisha nguma pini
Mjengoni wasikae kinyonge

Anaitwa Roma hakuna wa kumstopisha Roma Roma
Nani wa kunyamazisha Roma Roma
Kazi kuongea ongea kesho yake on air
Kesho kutwa wamepotea 

Anaitwa Roma hakuna wa kumstopisha
Nani wa kunyamazisha Roma Roma
Kazi kuongea ongea kesho yake on air
Kesho kutwa wamepotea 

Watch Video

About Anaitwa Roma

Album : Anaitwa Roma (Single)
Release Year : 2019
Copyright : (c) 2019
Added By : Huntyr Kelx
Published : Nov 15 , 2019

More ROMA Lyrics

ROMA
ROMA
ROMA
ROMA

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl