ROMA Zibambwe cover image

Zibambwe Lyrics

Zibambwe Lyrics by ROMA


Tongwe records
Bin laden (Oooooh) 
Geof Master (ooooh)

Wengi mlijiuliza walioniteka ni maaskari
Mkanitafuta vituo vyote Central hadi Sitaki Shari
Wakasema hawajui nilipo mama alienda hadi mortuary 
Dah! Ya Kaisari muachie Kaisari

Machozi yenu yatalipwa 
Mi nafunga na kusali
Imba Roma imba, imba Roma imba
Imba Roma imba

Mungu wa Paulo, ndo Mungu ungu wa Daudi
Na ndo Mungu wa John mnaemuita Yohana wa Yahudi
Mwanangu alimuuliza mama baba lini atarudi
Na mke wangu aliwaliza kuwashukuru sina budi

Fahamu ya kuwa mi sio tu rappa, mi ni baba wa familia
Na watoto mahitaji nawapa kama isemavyo Biblia
Kipi bora? Nife mseme nilikufa kiharakati?
Siogopi kufa, ila nawaachaje wanaobaki?

Je, nani kati yenu mwanangu atampa malezi?
Wapi atapata mahitaji, wapi atapata mapenzi?
Mama nae wapi atapata mahitaji na malezi?
Na ripoti ya upelelezi vipi akiiteka mtekaji?

Je kaburi langu mtalipalilia majani?
Nimeumwa hamjakuja niona mnangoja mje msibani
Nilipokuwepo sikuwa najua hii saa nne, hii saa nane
Nilichohitaji nitoke mzima na ndugu zangu tuonane

Nimechapwa mijeledi, nimevunjwa bila huruma
Asante mliopaza sauti nmeiona nguvu ya umma
Siku tatu nimefungwa macho
Mikono imefungwa nyuma (Mikono imefungwa nyuma)

Nakwenda Zimbabwe, simama iyelele mama wee
Nakwenda Zimbabwe, simama iyelele mama wee
Nakwenda Zimbabwe, simama iyelele mama wee
Nakwenda Zimbabwe, simama iyelele mama wee

Imba Roma imbaaa (oooh)
Eeeh Roma, sema baba weeeh

Nasimama na naunga hoja kwenye uchumi wa viwanda
Nanasi linaoza mzoga tikiti linaoza shamba
Waloniteka hawakuja na Noah, ni uvumi na visanga
Ila kutekana tekana huu ni uhuni wa kishamba

Weka bunduki chini si tubishane kwa hoja
Maana sote lengo letu kuijenga Tanzania moja
Mi sikuona nyota kwa shoulder ila najua we ni soldier
Inshaallah, ulikuja mwenyewe ama ulipewa order?

Aminini siku hazigandi
We ni Yanga mi Simba kuwa mpinzani sio dhambi
Ipo siku mtawala atakua mpinzani
Simba akichukia kombe sijui atapona nani?

Na kuna mbunge alisema eti nimemtukana mkuu
Utahukumiwa na mkono wa Mungu, namshitakia alie juu
Kwanza lini na kwaninii nimtukane mjomba?
Umepewa gari ya wagonjwa mi Tanga ananijengea bomba

Mi mbarikiwa na nikifa kuume kwa baba ntaketi
Na mtu wa watu that's why lilisimama bunge la bajeti
Kunijadili mtanzania kuwa makini pia
Makinikia nayatungia mapini pia

Nilitabiri utaitwa raisi kipindi unaitwa waziri
Japo maisha sio rahisi ila pongezi unastahili
Na waliosadiki Roma ataonekana kabla ya Jumapili
God bless imetimia injiri niliyoitabiri

Nakwenda Zimbabwe, simama iyelele mama wee
Nakwenda Zimbabwe, simama iyelele mama wee
Nakwenda Zimbabwe, simama iyelele mama wee
Nakwenda Zimbabwe, simama iyelele mama wee

Imba Roma
Eeeeeeh Roma, simama simama
Oyoyoyo eeeeeh Roma 
Sema baba wee

Iyelele mama wee, wee nakwenda
Wee Zimbabwe
Iyelele mama wee, mama wee
Ooooh

Watch Video

About Zibambwe

Album : Zibambwe
Release Year : 2017
Copyright : (c) 2017
Added By : Huntyr Kelx
Published : Apr 26 , 2020

More ROMA Lyrics

ROMA
ROMA
ROMA

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl