NACHA Mnachangaya cover image

Mnachangaya Lyrics

Mnachangaya Lyrics by NACHA


yasubi ndani ya mbanyu
 
Habari ndugu zangu marafiki jamaah
Nimesimama hapa kuwakilisha mtaa
Kwa usahihi na ufasaha mimi naitwa Nacha
Almaarufu Sandi Manara naamini mnanipata
 
Taarifa njema kwamba nimealikwa na mzee
Mimi na yeye meza moja tuongee
Okey, usilete mambo ya uoga
Mtaani ni kugumu, kutwa tunakula zoga
 
Mmmh, kugumu kivipi? Kutwa mnabeti
Instagramu peji zenu, picha za uchi mnaposti
Wasanii kufungiwa kucha kutwa yaani nuksi
Tatizo wasanii na nyinyi daily matusi
 
Madada wanaojiuza huku danguroni
Ah-ah, mimi siwezi kuongea na mzee mambo ya kihuni
Madawa hospitali, eeh hilo nitamwambia
Viwanda alivyosema, hilo nitamwambia pia
Wabunge kutukana bungeni bila siri
Siwezi kusema kuna kamati ya maadili
Hmmh, jeti neki hio ndo balaa
Mi siwezi nikasema, nyie mnataka nihame Dar

Aaah, eeh mbona mnachanganya
Unatoka wapi urafiki wa paka panya
Aaaah, ah kumbe tunaelewana
Kakwambia nani undugu ni kufanana

Aaaah, mbona mnachanganya
Unatoka wapi urafiki wa paka panya
Aaaah, kumbe mnaelewana
Kakwambia nani undugu ni kufanana

Naam, madawa yanaharibu wanamziki
Hamsaidie mtoto ila anayaahidi
Ashasaidiwa na bado hashikiki
Nimeamini kweli kunguru hafungiki

Mi nilitegemea labda mtakuwa na hamu
Kwanini Bongo kichwa cha mwendawazimu
Hamna kazi na mmesoma mpaka chuo
Vikasa vipo wapi kama elimu ni ufunguo

Tajwa mboga mboga, ushuru kwenye koo
Uswazi mvua zikinyesha wanazibua vyoo
Ah, ihalalishwe bangi, acheni akili za kizembe
Hivi mnajua, ya kuwa, shujaa jing'ua
Zina madhara kwenu, tena sanaa
Mwisho ya yote nitapiga naye selfie
Nikaposti Insta kwangu na peji ni private

Okey, nadhani tumeelewana
Kila mmoja wetu ana majukumu ya kufanya
Utawasilisha vile vyote vyenye maana
Ushindi wetu ni umoja pamoja waungwana

Aaah, eeh mbona mnachanganya
Unatoka wapi urafiki wa paka panya
Aaaah, ah kumbe tunaelewana
Kakwambia nani undugu ni kufanana

Aaaah, mbona mnachanganya
Unatoka wapi urafiki wa paka panya
Aaaah, kumbe mnaelewana
Kakwambia nani undugu ni kufanana

Watch Video

About Mnachangaya

Album : Mnachangaya (Single)
Release Year : 2019
Added By : Huntyr Kelx
Published : Aug 20 , 2019

More NACHA Lyrics

NACHA
NACHA
NACHA
NACHA

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl