DIZASTA VINA A confession of a Mad Philosopher cover image

A confession of a Mad Philosopher Lyrics

A confession of a Mad Philosopher Lyrics by DIZASTA VINA


Maana ya uhuru huisha baada ya utambuzi
Baada ya kutambua kwamba uhuru si maamuzi
Maana Kifungo na mipaka vinafanana
Aliyekuambia kuna uhuru utaupata kakudanganya
Ipo asili inayofanya mwili wako mashine
Kufanya Ugonjwa uwe jela alafu afya ni jela nyingine
Mjamaa amemwaga damu tayari
Awe huru ili akawe mtumwa kwa mabepari
Chagua kufa ukiona waja hawalipi wema
Kufa wokovu kilichokufa hakifi tena
Kufa ni uhuru kamili tabu ni nini
Haupo huru sasa uhuru wa kweli ni kaburini
Unakumbatia uhuru wa kuambiwa
Wakati unaishi na haukuchagua kuzaliwa
Uhuru hautafutwi msafiri pumzika kubali chai
Hauwezi kuwa huru ungali hai
Uhuru si halisi jamaa badili umbo
Uhuru sio jibu hata usikariri fumbo
Uhuru ni falsafa ya vitabu iliandikwa na mababu
Tutaisoma na mwisho itabaki huko
Anayehitaji uhuru aelewe
Kuogopa kufa ni utumwa kwa maana kufa ndio uhuru wenyewe
Hata uwe mfalme ambaye anatoa idhini
Huwei kuwa huru uhuru wa kweli ni kaburini

Freedom (freedom)
Freedom (freedom)
Freedom (freedom)
Freedom (freedom)

Ukikumbatia mwanga jua utaificha nuru
Uhuru si kwa mwafrika kumkimbiza mkabulu
Kuutaka uhuru sana jamaa si dalili njema
Kama upo hai na unahisi uko huru fikiri tena
Cheo huleta nuru pahala nuru haifiki
Na pesa ndio njia ya uhuru ukiimiliki
Pesa na cheo upita kule hakuingiliki
Alisema mlevi mmoja ambaye pombe tu imemdhibiti
Mwathirika ambaye dawa za kulevya zimefunga
Na anahisi yuko huru mara baada tu ya kuvuta
Labda si kweli haupo huru ukijiongeza
Maana ukishaujua uhuru tayari ushaupoteza
Je utaniona chizi au mwivi
Au pumbavu au mshenzi ninayeongea vituko
Au utaamua ukae chini utafakari
kisha ukakubali ndoa ajira navyo pia vifungo
Aliye huru ni nani nieleze mtoto anayeenda kwa viboko
Au mlokole mtenda mema baada ya kutishiwa moto
Au msomi elimu mpaka chuo kihakiki
I swera kama uhuru ndio huo siuafiki
Anayehisi yuko huru pita mbele
Piga kelele maana hata Mungu wako hayuko huru
Hawezi kubadili mipango hawezi kumuumba
Mungu mwingine mkubwa kupita yeye
Unaetafuta uhuru wa kweli utateseka
Utapoteza damu utatoa machozi na utakesha
Hauwezi kuupata maana hakuna ulipouweka
Uhuru haupatikani kwa fedha
Uhuru is priceless kwakuwa si bidhaa halisi
Wenye chapaa walihakiki
Utaniangusha sana ukishindwa kuamini
Upo uhuru  ila uhuru wa kweli ni kaburini

You don’t have freedom
You can have freedom
You don’t have freedom
You can have freedom
Freedom (freedom)
Freedom (freedom)
Freedom (freedom)
Freedom (freedom)

Watch Video

About A confession of a Mad Philosopher

Album : The Verteller (Album)
Release Year : 2023
Added By : Farida
Published : Jun 17 , 2023

More DIZASTA VINA Lyrics

DIZASTA VINA
DIZASTA VINA
DIZASTA VINA

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl