Darasa Lyrics by BANDO


Ah! Nikiwa na hasira
Wa kunituliza simuoni
Naweza nikakunja ndita 
Alafu nikaziweka mfukoni
Ni kweli sina bei
Ila nina uwezo wa kumpa "Hi" Mond
Alafu nisimpe salamu SK

Wapinzani wanagwaya navyotisha
Unapomwita dem wangu malaya 
Basi hakikisha dadako bikra
Leta mizinguo kwa mkupuo
Hapo ndo utajua kwamba luku 
Haina kifurushi cha chuo

Si hatushindani kuvaa
Tunasaka chapaa
Eti mganga hajigangi
Mbona nimeshaganga sana njaa

Nisikize we jamaa
Ukibisha nitashangaa
Mlimani city ndo mlima pekee
Unaopatikana Dar

Mambo ya vichwa haya
Dah! Ni mikosi
Hivi mnajua kichwa cha chini 
Hakinaga utosi

Mi mwenzako mambo ya vumbi
Sitaki kuyajua
Nishapaka vumbi la Congo
Likanipa tu mafua 

Asa na waambie na wenzenu
Leo yule kiziwi kajiskia
Yule mkali wenu ambaye 
Hata Ebitoke anamhofia
Sema ugomvi huwa sitaki
Nikiwa na hasira alafu 
Nikakosa cha kupiga 
Mi huwaga hupiga mswaki

Mfanya mapenzi juu ya ndege ni mhuni
Tena uhuni uliobobea 
Maana dhambi nawahi kufika mbinguni
Ila kambi popote fuata pay
Diwani utaongoza kata zote ila sio kata K

Ukilala fofo, hupati pay
Soko, hupandi bei
Local, mtoko international, hupati "Hey"
Koko, no say, kubweka, push Nay
Stori za wanoko, ni michosho kila day

Kaka I am sorry kuuliza sio umbezi
Hivi kati ya Country Boy na Shilole
Unadhani yupi Mnyamwezi?
Mmmh usiniulize hayo maswali ya ki-
Kati ya Msukule msukuma nani ni msukuma?

Mama watoto, avaliwe au nipite kama mpoto
Ndani pamoto, changamoto kuna kipindi
Tulikosa chakula tukala msoto

Huwa nikimuona mrembo amesimama dede
Na niliona Yesu bwana anasema bwana ni bebe
Si unajua mi ni rasta kama Chege
Ni sawa na Alikiba kuvaa buti la jeje

Hapa Bongo nahisi soccer hakuna
Bando nikiamua kufanya soccer 
Nitafanya guna hadi ole guna
Kwenye tungo mi nafahamu 
Nikifa nitaacha upendo
Nishajiuliza kibogoyo akifa
Ataacha pengo?

Na siku hizi niko busy na mapene
So madem zenu vichwa panzi mwili senene
Na hii hali nakondesha kishenzi
Wenzako wanaendesha magari 
We unaendeshwa na mapenzi

Mimi ndo kiboko 
Ya hawa madogo wanaofoka foka
Suti inanukia majani
So jua namoka moka

Salamu mpeeni Sanchoka
Mwaambieni akimwaga radhi
Akianani naziokota 

Ah swala linaponiskia huhofia jibu
Si wamekosa vya kutia wameamua kutia aibu
Waambie na walo nipania hata kizibo
Ni mfuniko ila hatuwezi kufunika sufuria

I say ni kisanga
Leo maiti imebeba jeneza
Mwenye kiti leo amebeba na meza
Mchezo unahitaji fikra
Bongo movie walivyo waongo
Unaweza kuta Uwoya kaigiza bikra

Watch Video

About Darasa

Album : Darasa (Single)
Release Year : 2020
Copyright : (c) 2020
Added By : Huntyr Kelx
Published : Aug 08 , 2020

More BANDO Lyrics

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl