NACHA Grow Up cover image

Grow Up Lyrics

Grow Up Lyrics by NACHA


(Kiri)

Ladies and Gentlemen
I go by the name N.A.C.H.A aka Nacha
Mnyasubi ndani ya mbanyu beiby

Asante Mungu kwa kunipa pumzi ambayo silipii ushuru
Nisipokushukuru ni dhahiri moja kwa moja nakukufuru
Asante kwa kunipa nafasi ya kuongea na wanao nisikiliza
Ili nijue kama wameshakuwa au wanahitaji 
Kumwagiliziwa mbolea ili kukua

Tunahitaji kugrow up maana tuna akili finyu kwa kuwa
Tunaweza kulipia hoteli elfu hamsini
Kufanya sex alafu condom ni ya mia tano tu
Ikatushinda kununua, nobody care
GROW UP!

Ajira zimekuwa ngumu 
Kaka yangu kahitimu chuo kikuu cha Dar es Salaam
Kaamua kujikita kwenye michezo ya kubahatisha
Swali ni je? Kubet ndio kitu alisomea 
Kutoka Standard One mpaka chuo?
GROW UP aisee wavalisheni nguo

Mi huwanga sichukuliangi vitu personal though
Kuna mtangazaji aliyesema kumpa Nacha interview 
Ni mpaka awe na demand mtaani
Question hiyo demand nitaipata vipi 
Wakati nahitaji kusupportiwa ili niwe na hiyo demand mtaani 
Yaani ni sawa na mtu kutoka chuo na kuomba kazi 
Alafu unamwambia ni lazima awe na uzoefu wa hiyo kazi
Nonsense!

Sababu za kiintelejesia 
Utapasuka msamba ukijaribu kuwaiga
Na ukijaribu tu kuupaza tu sauti na kuwauliza 
Kwa nini nyinyi mnakula vya juu?
Watakujibu tunakula vya juu 
Kwa sababu tuna shingo za twiga(Mschew)

Huo ni ubinafsi ulafi na uchoyo 
Wa kutaka wao pekee yao
Na ndugu zao mikono yao iende kinywani
Alafu mikono yako iende shavuni
Take care GROW UP!

Bado nawashangaa wadau wa kandanda Bongo
Kukiponda chama cha mpira cha nchi hii kiko ovyo
Eti tu kisa National team haijafuzu World Cup ama AFCON
Nina swali nataka majibu sio kingine

Serikali inasupport soka kama sekta nyeti zingine
Je tuna waalimu wenye taluma 
Na leseni za juu kutoka FIFA?
Na je shuleni michezo ni lazima 
Kwa maana umeitashume tena umeseta

Na mwisho kabisa 
Nchi yako ina viwanja bora na academy za kutosha 
Big NO definitely
Mafanikio ya chochote ni maandalizi toka chini
Acheni kuchekesha GROW UP!

Nilichoamua ni kumwamini Mungu tu 
Ila kumwamini mwanadamu mwenzangu sitaki
Tena huo ni unafiki 
Mtumishi wa mungu kutufundisha mema 
Huku kwa simu yake kajaza pornography
Wizi, GROW UP!

Mnadhani nawahofia? Hapana 
Msichokijua ni kuwa nahofia anopheles
Ndio maana kabla ya kulala nakishukisha chandarua
Na nangoja tu niwajuze
Wa kumsimamisha roma sio stamina
Ni Napoly, Inter Milan au Juve trust me

Kibaya ni kuwa tumezaliwa 
Kwenye nchi ambayo wasomi wako mtaani
Ndio maana mi niliamua tu 
Kuingia madrasa kuhifadhi Bible na Quran
 
Kizazi cha fall kizazi cha Instagram
Kizazi cha facebook, kizazi cha WhatsApp
Kizazi cha Twitter, kizazi cha Telegram
Kizazi cha Smartphone, make-up na fashion 
Za kim kardashian na Migos ndio kizazi cha vigoma
Na ndio kizazi cha zero nadhani wote mnakiona 
Na ndio maana kila siku tutazidi 
Kuzalisha akina Amber Ruty wengi
Tena under age kuitaka ndoa 
Wakati huwezi kumpikia hata mume uji

Muungwana humpongeza muungwana akifanya vya maana
Watumishi hewa walifyekwa safi 
Barabara safi, treni ya mwendo kasi na fly over
Bado tu serikali ya viwanda, ajira kwa vijana
Kupanda mishahara kwa walimu na polisi
Ndio vitu tunavyoongoja

Tumeitupa Bongo fleva na kuiga sound ya Nigeria
Au mi ndo sijajuwa pengine 
Bongo fleva is a type of Nigerian music, I don’t know
Mpaka sasa mtaani ni msoto 
Na sijakutana na what is Biology?
Mpaka naamini huo ni uzushi 
Labda study za kazi 
Kidogo imenisaidia kuwa fundi Washi

Bahati mbaya mi sio mwarabu sina kitu cha kurithi
Mtaniua bure babangu ni masikini, mamangu ni masikini
Na hata kwetu kijijini nilichoachiwa 
Sio mali za ng’ombe sabini
Ila nimeachiwa utajiri kichwani 
Kuwa this time tomorrow ni past like a shadow
GROW UP!

Ubinafsi ndio kitu nilicho nyimwa 
Nyinyi si mlizipandisha na muungo wa Utuhui Stars
Njombe Mji Lipuli, Maji Maji na Ndanda 
Mimi nitazipandisha Nyasubi FC, Kahama United
Stand United, Mbanga FC, Rhino Rangers
Toto Africans, Pamba na Gwambira

Guess what? 
Mi sikuzaliwa nje ya ndoa, La hasha 
Ndio maana nawaheshimu sana wanawake
Ndio maana naogopa kuwachezea na kuwazalisha 
Na kuwatelekeza na niishie kuwatia
Yaani kuwatia dosari na kuwatia doa
 
Asa kumbe hata iwe ni msoto 
Iwe changamoto rijali hakatai mtoto
Mkamatwa na ngozi si ndio mla nyama
Asa mbona mnawahanya?

Mwenyekiti wa chama tawala na mgogoro 
Mzito na mwenyekiti wa chama pinzani(Mschweeew)
Jamani punguzeni ushabiki kitu haukijui unakausha
Maana sisi hasa wengi wetu hatuna uelewa kuhusu siasa

Sijajuwa ni uzembe wa mzazi 
Uuzembe wa walimu au ni mfumo wa elimu
Ndio unasababisha kumkuta mtoto wa darasa la tano 
Hajui kusoma wala kuandika, globalization

Mtakuwa wajinga mpaka lini? 
Kuunga megabytes kwa ajili ya kufuatilia 
Udaku, picha chafu za video za Sanchoka
Nagundua tunapokwenda ni mbali sana kuliko tulipotoka
GROW UP!

Ni utandawazi au ni uzembe ulifanywa na wazazi
Sasa ivi ni kawaida kumkuta kijana 
Mwenye umri wa miaka thelathini 
Kuishi kwa wazazi
GROW UP! 

Nawawashia green lights 
Taifa la mbumbumbu kushadadia mambo
Na ndo maana kwenye ngoma serious 
Kama hizi utakuta dislikes

Kuwasaida hawa sio kuwapa laki mbili 
Bali kuwasaidia hawa ni kuwafanyia counselling ya akili
Kabla ya kupigana kutukanana huwa 
Nageuka nyuma najiuliza mi ni nani? Nimetoka wapi?
Ndoto zangu zipi? 
Naweka silaha chini na kuwa mpole kwa maana
Mjini sina cha shangazi Sinza wala mjomba kwa Mtogole
Ako na watu sai wanajiuliza kwa nini Nacha hahiti
Kwa nini Nacha hawi star 
Na mawe yake yanapendwa sana kwa mtaa
Nawajibu mi ni mwezi kamwe siwezi kuwa star

Guess what? 
Wanawake wa sasa ingawa sio wote 
Ila wengi wao wana tamaa
Hawana kinyaa wanameza matapishi 
Ambayo rafiki yake kayakataa
Na ndio maana wanazidi kuambukizana 
Moto sababu ya motor car

Na ndio maana vijana wengi sai 
Wanatumia muda mwingi kujiremba kama mabinti
Kuwa smart kutafuta majimama ni true sio masihara 
Kuliko kutumia muda mwingi kutafuta kazi 
Wapate ugali ili wawe wanaenda chooni mara kwa mara
GROW UP!

Asanteni naitwa NACHA

(Bear)

Watch Video

About Grow Up

Album : Grow Up (Single)
Release Year : 2020
Copyright : (c) 2020
Added By : Huntyr Kelx
Published : Feb 21 , 2020

More NACHA Lyrics

NACHA
NACHA
NACHA
NACHA

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl