Chama la Wana Lyrics by BANDO


Mnyamwezi nimeshanyuka pamba
Sembuse kuwanyuka nyie watoto
Madem, vicheche mnaozunguka juu ya moto
Bila hela ni vichomi
Dem wako akilala na dera 
Jua kuna mtu anaenda kuchambua ndotoni

Mapenzi ya siku hizi kama hiari
Wengi tunaishi tegeta nyuki 
Ila hatujui utamu wa asali
Watacho kwambia we usijali
Maana huwezi kutumia kamba ya rubber
Kukazia buti gari

Wa Makonde ndo anashabikia danda 
Unaezakuta mkude simba anae anashabikia Yanga
Wanaposema mi ni mkali nazidisha gundu
Mwislamu ana swali ila anahisi jibu analo Mungu

Oh my God!Kasali vipi usawa unabana
Naliskia eti mchungaji amekula kondoo wa bwana
Yaani noma sana, dunia Dar, ulimwengu shujaa
Ushai jiuliza hivi kipofu naye anaona kinyaa?

Sioni ajabu, mshamba akinyoa denge
Ni ajabu sana kuona hadi mamba kaingia mkenge
Hali ngumu kila sehemu
Ila pesa ndo bwana pekee ambaye anadumu na kila dem

Dusco dusco bado nyie hamjui kurap mnazuga
Dusco dusco bado mi ndo yule champion kila muda
Mi ni chama la wana, hawajui kama chama la wana
Mi ni chama la wana, hawajui mi ni chama la wana

Dusco dusco bado nyie hamjui kurap mnazuga
Dusco dusco bado mi ndo yule champion kila muda
Mi ni chama la wana, hawajui kama chama la wana
Mi ni chama la wana, hawajui mi ni chama la wana

Aah mamlaka ya hali ya hewa inanisaka na rabii
Eti nachafua anga, navyotema hizi fasihi
Navyo saga hizi laini utasema nina ubongo wa blader
Seremala, yule chonga kitu moto mnachopenda 

Kifupi sili chungwa na maganda 
Dem wangu guitar maana dem amesave kinanda
Hii serikali ya viwanda, inanipa ndoto mbevu
Nyumbani nimeshajenga banda, nina dream ya kufunga ndevu

Siwezi lala na njaa, nitalala na wife
Ukiona nimeshika kitanzi, ujue nalala na life
Akili ni nywele nachokiwaza kiko mbali
Bonya kipilipili ndo ana akili ya kachumbari

Ah mziki wito wengi wanachana ila hawana sifa
Mchezo simple dana dana ila hauhitaji keeper 
Utani mwiko, nilipo hauwezi figure
Unaweza ukawa fundi jiko na bado usijuwe kupika 

Dusco dusco bado nyie hamjui kurap mnazuga
Dusco dusco bado mi ndo yule champion kila muda
Mi ni chama la wana, hawajui kama chama la wana
Mi ni chama la wana, hawajui mi ni chama la wana

Dusco dusco bado nyie hamjui kurap mnazuga
Dusco dusco bado mi ndo yule champion kila muda
Mi ni chama la wana, hawajui kama chama la wana
Mi ni chama la wana, hawajui mi ni chama la wana

Ah, na mapigo ya kila style tae kwon ndo mpaka kung fu
Hadi -- naipakia buturu
Sasa twanga ukoboe usikodoe
Naposema akili nywele, niambie ni za wapi ili nizinyoe

Am sorry brother, maisha safari isiyo na traffiki
Wanaofika kileleni, gari wanapandiaga wapi?
Sepeni vya ndenzo, mi ni yule Ustadh Bishoo 
Mpaka kanzu naivalia mlegezo

Asiye nijua, mwambieni mi ni hatari kwake
Tena hatari sana, shubiri mkewe ni asali kwake
Dem wako ana habari zake?
Ndo yule jamaa mlafi ambaye anakula chakula na mpishi wake

Dusco dusco bado nyie hamjui kurap mnazuga
Dusco dusco bado mi ndo yule champion kila muda
Mi ni chama la wana, hawajui kama chama la wana
Mi ni chama la wana, hawajui mi ni chama la wana

Dusco dusco bado nyie hamjui kurap mnazuga
Dusco dusco bado mi ndo yule champion kila muda
Mi ni chama la wana, hawajui kama chama la wana
Mi ni chama la wana, hawajui mi ni chama la wana

Watch Video

About Chama la Wana

Album : Chama la Wana (Single)
Release Year : 2019
Copyright : (c)2019
Added By : Huntyr Kelx
Published : Aug 01 , 2019

More BANDO Lyrics

BANDO
BANDO
BANDO

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl