Hatua kwa Hatua Lyrics by REBEKAH DAWN


Sauti nyingi zinanizingira
Mawaitha mingi, njia nyingi
Lakini najua Sauti moja tu la kufuata
Sina Mchungaji mwingine ila Yesu

Hata wengine wakiteleza njiani
Nitazidi kuwa mwaminifu Kwake
Nitaamini neno Lake
Hajawahi kunipotosha

Hatua kwa hatua, nitaendelea
Mungu mbele yangu, nitamfuata
Hakuna njia ingine najua
Hatua kwa hatua, nitaendelea

Njia zake zaaminika
Neno lake ni la kweli
Kwa hilo nitasimama
Sitainamia dunia
Sina Mwongozo mwingine ila Yesu

Sijawahi ona mwenye haki ameachwa
Waliokuchagua hawajawahi kujuta
Kwa hivyo nitazidii Nawe, hata nisipoelewa

Hatua kwa hatua, nitaendelea
Mungu mbele yangu, nitamfuata
Hakuna njia ingine najua
Hatua kwa hatua, nitaendelea

Oooh, nitakufuata
Nitakufuata Yesu, Kiongozi mwema

Mkombozi, sina mwingine
Mfalme, sina mwingine
Mwenye Enzi, sina mwingine
Msaidizi, sina mwingine
Mponyaji, sina mwingine
Mtetezi, sina mwingine
Mwokozi, sina mwingine
Mfariji, sina mwingine

Hatua kwa hatua, nitaendelea
Mungu mbele yangu, nitamfuata
Hakuna njia ingine najua
Hatua kwa hatua, nitaendelea

Watch Video

About Hatua kwa Hatua

Album : Hatua kwa Hatua (Single)
Release Year : 2021
Copyright : (c) 2021
Added By : Huntyr Kelx
Published : Sep 29 , 2021

More REBEKAH DAWN Lyrics

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl