MR BLUE Nitabadilika cover image

Nitabadilika Lyrics

Nitabadilika Lyrics by MR BLUE


Nikitoka tungi, nikirudi tungi
Nguvumbi mdomoni kutu na merungi
Kete na makundi vicheche sijivungi
Siku inaishaga bar nikilala kila ukumbi

Alfajiri ikifika ndo narudi
Nimekasirika nimekunja ndita
Sorry mama sipendi kukuudhi
Mambo ya ujana na nitabadilika

Kabla ya kulala napiga goti kwa Allah
Kila siku ni sala kuiombea hii familia
Namwomba Mola hili kapu litie fora
Nyumbani maisha bora na ndani wainuke bora

Mimi ni binadamu mama sijakamilika
Hizi kero ndogo ndogo sawa nitabadilika 
Najua unanijua lile penzi nalokupa
Zawadi yako ni mimi usinuitenge kisa chupa

Nachopata ni kidogo ila chote nakupa wewe
Nakutunza kwa chakula na ukitaka pombe ulewe
Vumilia hii tabia hela zote nakunywa bia
Kuna siku nitatulia na masikio yatakusikia

Koma na mimi
Shida ndogo ndogo nisitiri
Kwa kulea watoto ni mimi nawe
We na mimi 

Koma na mimi
Shida ndogo ndogo nisitiri
Kwa kulea watoto ni mimi nawe
We na mimi 

Muda wake ni kidogo tu
Muda mwingi marafiki
Muda mwingi kwenye mziki
Muda kutafta riziki
Muda kutafta makiki
Muda wa kumtafuta shabiki
Muda(Muda)

Awali haikuwa hivi
Rafiki wananiuliza kheri umekuwa chizi?
Na mimi ndo nawajib, Mbona mnakuwa hivi?
Hamjui kama chizi hajijui akiwa chizi?

Hata nikupe malazi makasi
Lazima utatafuta penzi letu lilipo
Na mi ninakuweka wazi
Sheria ya kwanza ni harusi na inayofuata ni kifo

Ibilisi na shetani umeniganda
Umenifanya kama gasi mtoto wa watu unanipanda
Ona nananana nitakutwa kutwa kwenye ubanda
Shemeji mchawi, mke namwona mwanga

Kama kuna jitu limeniendea kwa mganga
Dah! Mi mwenyewe naumia 
Ita bia hela zote nakunywa bia
Kuna siku nitatulia, na masikio yatakusikia

Koma na mimi
Shida ndogo ndogo nisitiri
Kwa kulea watoto ni mimi nawe
We na mimi 

Koma na mimi
Shida ndogo ndogo nisitiri
Kwa kulea watoto ni mimi nawe
We na mimi 

Nitabadilika, nitabadilika
Nitabadilika, nitabadilika

Watch Video

About Nitabadilika

Album : Nitabadilika (Single)
Release Year : 2019
Copyright : (c) 2019
Added By : Huntyr Kelx
Published : Oct 16 , 2019

More MR BLUE Lyrics

MR BLUE
MR BLUE
MR BLUE
MR BLUE

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl