GLORIA MULIRO Narudisha cover image

Narudisha Lyrics

Narudisha Lyrics by GLORIA MULIRO


Abudiwa Bwana, tukuka Bwana,
Heshimika Bwana, tukuka milele,
Wewe ni Mungu hakuna kama wewe Bwana,
Unayotenda hakuna mwingine awezaye tenda,
Unarudishia watu miaka yao, waliopoteza
Ulimrudishia Ayubu miaka yote aliopoteza,
Mali yake watoto wote bwana ulirudisha,
Tena maradufu,
Miaka yangu iliyoliwa na nzige,

Bwana ulirudisha nami najua nitarudishiwa,
Miaka yangu nitarudishiwa,
Iliyoliwa na nzige nitarudisha,
Eeeiee miaka yangu,
Iliyoliwa na nzige,

Narudisha! narudisha!
Miaka yangu iliyoliwa na nzige,
Narudisha kwa jina la Yesu
Miaka yangu, iliyoliwa na nzige,
Narudisha kwa jina la Yesu.

Nzige wamekula amani ya wengi,
Nzige wameharibu afya ya wengi mno,
Angalia imebaki mifupa mikavu,
Tazama imebakia mifupa mikavu,
Lakini kuna tumaini, Bwana atarudisha,
Amani itarudishwa, afya itarudishwa,
Biashara itarudishwa, furaha inarudishwa,
Waliopakwa tope, Bwana anasafisha,
Walioshushwa chini Bwana anainua,
Ata mti ukikatwa, utachipuka tena,
Waliopoteza maono yao jipe moyo,
Bwana anarudisha kwa jina la yesu

Narudisha, narudisha,
Miaka yangu, iliyoliwa na nzige,
Narudisha kwa jina la Yesu,
Miaka yangu iliyoliwa na nzige,
Narudisha kwa jina la Yesu.

Watch Video

About Narudisha

Album : Narudisha (Single)
Release Year : 2017
Copyright : ©2017
Added By : Trendy Sushi
Published : Feb 10 , 2020

More GLORIA MULIRO Lyrics

GLORIA MULIRO
GLORIA MULIRO
GLORIA MULIRO
GLORIA MULIRO

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl