...

Paroles de Dunia Par HANSTONE


Mi mwenyewe mtoto, mi ningali motto

Nakinga jahazi lisije kuzama maana maji ya ugoko

Nyingi changamoto, kuifikia ndoto

Najichunga nisije ungua, na ujana maji ya moto

Hata ujipange dunia (dunia), nani alikuambia?

Naomba uyasikie siku ya mwisho, wanayosema hata usiowadhania

Utacheka, utalia. Haina mzani dunia

Wapo wanaoomba uteseke. (Aaaaah aaah)

Kasema baba nsifuate dunia

Aliniambia mama nisifuate dunia (Aaaah)

Alisema bibi kaiacha dunia

Na wewe utasema utaiaga dunia (Ooooh)

Jamani dunia. Ooooh dunia. Aaaah dunia

Ooooh dunia. Lisemwa. Lisemwa (Oh)

Lisemwalo lipo, kama halipo basi laja

Yalisemwa (Oooh). Yalinenwa (Oh)

Yanapozidi mateso, inakuja faraja (Aaaaah)

Oh, eti dunia duara

Kuna muda kama siamini

Naona kama imenyooka, tunapokwenda twaishia chini

Jamvi na mswala, turudi kwetu tunayemuamini

Usishangae rafiki anakua adui, kwa sababu ya aliye akilini (Mmmh)

Mwenye anacho, ambaye hana hathaminiki

Kwa tumachomacho, kwa kubaniana riziki

Kikulacho kinatafuna hata mbichimbichi

Yaani dunia bado hata ukilia haisaidii (Aaaaaaah aaaaaah)

Kasema baba nsifuate dunia

Aliniambia mama nsifuate dunia

Alisema bibi kaiacha dunia

Nawe utasema utaiaga dunia (Ooooh)

Chuki, chuki inaanzaga kwa upendo (Mmmh)

Mamluki watakusemasema sio matendo

Sa sijui, nimuamini yupi?

Yupi nimkabidhi upendo

Moyo wangu asije dilute, akanichanganya, waniroge, aniachie pengo. (Aah)

Dunia pana, dunia tambara bovu. Sijui ndo mwisho

Maulana, yanazidi maovu

Watu wanashindana kufanya michezo mibovu

Au hata kuhakikisha kidonda linabaki kovu

Aaah, dunia. Ooooh, dunia. Mmmh. Mmmh

Kupata mpaka uwe na roho mbaya, ndivyo 'navyosema

Hata Mungu pia hafundishi ubaya, wanautoa wapi tena?

Tisa mzuri ila moja baya, wanafuta yote mema

Wanaomba kuzaliwa mbwa ulaya, sio kujiombea mahali pema

Kwa wanadam, Mungu tukumbushe

Kama dunia safar, njiani unishushe

Oh baba, nami univushe

Na ya dunia ni majaribu, naomba uniepushe (Aaah)

Ecouter

A Propos de "Dunia"

Album : (Single)
Année de Sortie : 2025
Copyright :
Ajouté par : Kieran
Published : Jul 15 , 2025

Plus de Lyrics de HANSTONE

HANSTONE
HANSTONE
HANSTONE
HANSTONE

Commentaires ( 0 )

Aucun commentaire pour l'instant



A propos de AfrikaLyrics

Afrika Lyrics est la plus large collection de paroles de chansons et de traductions d’Afrique. Afrika Lyrics fournit les paroles des musiques de plus de 30 pays africains et des traductions de lyrics de plus de 10 langues africaines en français et en anglais.

Suivre Afrika Lyrics

© 2025, We Tell Africa Group Sarl