EMMANUEL MGOGO Neno Lako ni Kweli cover image

Paroles de Neno Lako ni Kweli

Paroles de Neno Lako ni Kweli Par EMMANUEL MGOGO


Ni kweli, ni kweli
Neno lako ni kweli
Ni kweli, ni kweli
Neno lako ni kweli

Nimedhibitisha wala sina mashaka 
Neno lako ni kweli
Nimedhibitisha wala sina mashaka 
Neno lako ni kweli

Ni kweli, ni kweli
Unaweza ni kweli
Ni kweli, ni kweli
Unaweza ni kweli 

Nimedhibitisha wala sina mashaka 
Unaweza ni kweli 
Nimedhibitisha wala sina mashaka 
Unaweza ni kweli 

Katikati ya kelele dunia ikitingisika
Wewe ni ngome yangu nitakuwa imara
Wakitangaza mauti unatangaza uzima
Wewe ni ufufuo na uzima 

Katikati ya kelele dunia ikitingisika
Wewe ni ngome yangu nitasimama imara
Wakitangaza mauti unatangaza uzima
Wewe ni ufufuo na uzima 

Neno lako moja latosha
Kuangamiza jeshi la adui
Na maneno ya wabaya na kuwatupa mbali

Katikati ya giza nene
Elimu na ujuzi vinaposhindwa
Neno lako ni nuru ing'aayo gizani

Wengi wakisema siwezi
Wewe ukisema naweza
Baba neno lako ni kweli

Na hata kama wengi wameshindwa
Na hata CV yangu haieleweki
Kwa neno lako mimi ni mshindi

Nimedhibitisha wala sina mashaka 
Neno lako ni kweli 
Nimedhibitisha wala sina mashaka 
Unaweza ni kweli 

Katikati ya jangwa nikiwa na kiu
Wewe wanipa maji mwambani 
Katikati ya jangwa mimi nikiona kiu
Wewe wanipa maji mwambani 

Hapo mwanzo ulikuwepo
Vyote vilifanyika 
Kwa neno lako Mungu
Pasipo neno hakuna chochote
Kilichofanya neno lako ni kweli

Shuhuda zako ni kweli
Wala haudanganyi neno lako ni kweli
Shuhuda zako ni kweli
Wewe haudanganyi neno lako ni kweli

Kwa neno, kwa neno lako mimi ni mshindi
Halleluyah, Halleluyah, Halleluyah Amen
Kwa neno lako nasimama imara 
Halleluyah, Halleluyah, Halleluyah Amen

Wewe waona taifa kubwa
Ndani yake aliye tasa
Ulimuita Ibrahimu baba wa mataifa
Akiwa hana mwana ulidhibitisha neno lako
Kwa mwanamke tasa akapata watoto

Ni jambo gani gumu linipate
Hata nisiamini neno lako
Nimelidhibitisha neno lako ni kweli
Wala sina mashaka nakuamini Mungu

Kwa neno, kwa neno lako mimi ni mshindi
Halleluyah, Halleluyah, Halleluyah Amen
Kwa neno lako nasimama imara 
Halleluyah, Halleluyah, Halleluyah Amen

Ecouter

A Propos de "Neno Lako ni Kweli"

Album : Neno Lako Ni Kweli (Single)
Année de Sortie : 2021
Copyright : (c) 2021
Ajouté par : Huntyr Kelx
Published : Jan 16 , 2021

Plus de Lyrics de EMMANUEL MGOGO

EMMANUEL MGOGO

Commentaires ( 0 )

Aucun commentaire pour l'instant



A propos de AfrikaLyrics

Afrika Lyrics est la plus large collection de paroles de chansons et de traductions d’Afrique. Afrika Lyrics fournit les paroles des musiques de plus de 30 pays africains et des traductions de lyrics de plus de 10 langues africaines en français et en anglais.

Suivre Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl