Pesa Lyrics by BUNDUKI


Yeah yeah, naanza hapo

Mi ndo pesa cheki navyo wasumbua akili
Hawalali kutwa wanakesha kunitafuta midili
Nawapeleka puta mpaka majasho yanatoka
Vikwapa vinawanuka wanipati navyotoka

Adimu kama nini sipatikani kirahisi 
Nasakwa hadi porini mimi ni shavu kwa polisi
Ukikamatwa unitoe mimi wengine wananiita rushwa
Nina majina mengi mimi chanzo cha kusaga kutupwa

Waovu wananitumia ni wadhuru watu wema
Na wema wananitumia nami natumika vyema
Moyoni inakuwa faraja, nasahaukisha machungu
Matatizoni ni raha pia ni shida kwenye uchungu
Ili unipate nieke vyema nitunze nikutunze
Usije sema sikusema, kamwe usinipuuze
Wapo wanaonuna wakinikosa visirani haviishi
Usinichokoze utaniponza mi ndo pesa kishawishi

Wananiita pesa, pesa, pesa yeah
Wananiita pesa, pesa, pesa yeah
Wengine waniita money pesa mulla, money
Wengine waniita money pesa mulla, money
(Wengine wananiita)

Ulizaliwa unanikuta na ukifa unaniacha 
Wote wananitafuta na si wote wanaonipata
Nakidhi mahitaji kwenye maamuzi mi ndio jaji
Simpendi mfujaji kurudi kwake sitaraji
Anaenidharau ananitupa anayenidhamini ananiokota
Ukinipoteza utanijuta usingizini utaniota
Nampenda mwenye malengo haijalishi vitendo
Wananitumia kama chambo bila mi hufanyi mambo

Ila ni ngumu kunimiliki sikupi uhakika
Nitakupa vipi kiki na daily unanitafuta
Wengine wananipata kiugumu wengine kirahisi
Wengine wanajihukumu wananihadithia ka hadithi
Pamoja wanaheshimika nikikutosa unadharaulika
Mi mwanako wanakonificha huwezi ona pata picha
Wanaozoea kunikamata wananipata kila saa
Wanaoningojea ni mtata kama Yesu alivyopaa 

Wananiita pesa, pesa, pesa yeah
Wananiita pesa, pesa, pesa yeah
Wengine waniita money pesa mulla, money
Wengine waniita money pesa mulla, money
(Wengine wananiita)

Hakuna saa unauliza kichwa itakuwaje bila pesa
Ukikata tamaa we kwisha ukiogopa maisha unajitesa
Heshima pesa sio maneno siku hizi dhamani kitwa
Haijalishi sherehe ya msumeno nami ndo kila kitu
Ndo nae kupa kiburi usteme kama mate 
Nakufanya unakuwa jeuri ukinikosa unakuwa mnyonge
Ujanja kuwa na pesa ongeza utaftaji uwe nazo
Bila malengo wanachekesha juhudi utegwa vikwazo
Ni ndoto kila mtu anaota maisha mazuri mipango
Sio ndoto unaota ukiokota ukishtuka hakuna chako

Ni sumu ni tahadhari silaha kwa binadamu
Ndo pesa hila habari sasa pata ufahamu
Maskini wananitamani niwe karibu yao 
Nisiwe mbali dhamani niwe tumaini lao
Matajiri ndo kabisa hawataki niwatoke
Nikiwatoka na wamekwisha wanadhani niko siku zote

Pesa, pesa, pesa yeah
Pesa, pesa, pesa yeah..

Wananiita pesa, pesa, pesa yeah
Wengine waniita money pesa mulla, money
Wengine waniita money pesa mulla, money
(Wengine wananiita)

Watch Video

About Pesa

Album : Pesa (Single)
Release Year : 2020
Copyright : (c) 2020 Rooftop Gang.
Added By : Huntyr Kelx
Published : Jan 13 , 2020

More BUNDUKI Lyrics

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl