Hila Zimevunjwa Lyrics by BERNARD MUKASA


Mungu alipopanga ukombozi
Kusudi kutuosha dhambi hizi
Akakubali kwamba ye'mwenyezi
Afe kifo kibaya kionezi
Mti wakamuwamba kama mwizi
Wakidhani ya kwamba ameshindwa

Amefufuka Bwana na mwokozi
Kazivunja hila za Lusiferi
Katukomboa wana wa mwenyezi
Twaimba ndiyo maana nyimbo nzuri

Mungu akakubali kuonewa
Hakuweka wakili kutetewa
Nguo bila hiari kavuliwa
Kapigwa misumari kazomewa
Akabaki kusali kuombea
Wauaji wapate msamaha

Amefufuka Bwana na mwokozi
Kazivunja hila za Lusiferi
Katukomboa wana wa mwenyezi
Twaimba ndiyo maana nyimbo nzuri

Mungu atufundisha kujitoa
Ya wengi maisha kuokoa
Na anatukumbusha kupokea
Yanayotutisha kumwendea
Tusije kukatisha njema nia
Ili kuyapisha ya dunia

Amefufuka Bwana na mwokozi
Kazivunja hila za Lusiferi
Katukomboa wana wa mwenyezi
Twaimba ndiyo maana nyimbo nzuri

Watch Video

About Hila Zimevunjwa

Album : Hila Zimevunjwa (Single)
Release Year : 2021
Added By : Farida
Published : Apr 07 , 2021

More BERNARD MUKASA Lyrics

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl