TANNAH Huu ni Moto cover image

Huu ni Moto Lyrics

Huu ni Moto Lyrics by TANNAH


Tanna ft Bright - Huu ni moto lyrics

Naona mnachekesha, upepo mnaupaka rangi
Mnaweka siku kwenye friji na hazigandi
Mnapagawa eeh, njaa baada ya shibe
Mnakesha kupika mawe na mnangoja yaive

Sihitaji kuendesha gari
Endesheni nyinyi maana mimi naendesha
Akili za makaka mjini
Usipoiva, utaula mbichi
Kamata mwizi maana mie sikamatiki

Ngoja kwanza(Aaah) msinishike
Dhamani ya kuku mpaka sikukuu ifike
Pata potea najua hutanielewa
Ni kama mwiba ulikoingia utatokea

Pumzi ndogo njiani wamekomea
Leo mnavunja mwiko na jungu limekolea
Kwenye hii beat ni mazishi msibane
Msiba hauna gharama marehemu kafia nyumbani

Huu ni moto, wa kuotea mbali 
Mtoko, na sitoweza haya
Ngoma ya kitoto, pole huwezi igiza kali 
Jibebe, jibebe

Mwendo kasi natia gear
Ukianza namalizia
Ngoma lisambe spidi mia
Ukiunga tela nakanyagia(Ona)

Sasa ipi mnataka? Nini mnataka?
Huu mchezo mbona simple
Pumzi za mrisho ngasa
Tannah ni Tannah, wewe ni wewe
Ingiza vifaranga ndani nakatiza mwewe

Am the winner nimepangwa na vibonde
Mnatoka makamasi mnagongana ka vikombe
Mtaa wa ambapo, nibebe
Kinondoni Tannah, TMK ni Chege
Nitachezesha reggea nitawalewesha mbege
Mtaanza kuona moshi kama disco la reggea

Watoto mwisho mtatokaga damu
Mtajikuta posta mnaamkia sanamu
Tannah na Bear moto hauzimi
Majembe ya nini sasa? Na mjini hatulimi
Jua ina giza aisee mtapotea
Mi Tannah ni bahari mtajikuta mnaelea

Huu ni moto, wa kuotea mbali 
Mtoko, na sitoweza haya
Ngoma ya kitoto, pole huwezi igiza kali 
Jibebe, jibebe

Mwendo kasi natia gear
Ukianza namalizia
Ngoma lisambe spidi mia
Ukiunga tela nakanyagia(Ona)

1,2 - 1,2 mi ndio matawi ya juu
Level chafu, busu nasi 
Mbona mtaa yalikuuma
Yaani sana tu, saana tu

Ushindi wa matuta kwenu afadhali
Namba saba kwenye bukta mjihadhari
Polepole bila pupa nawalaza chali
Kazi chobo chenga nawapiga dali

Zigizaga eeh, zigizaga
Nawashona zigizaga...

(Kiri Records)

 

Watch Video

About Huu ni Moto

Album : Huu ni Moto (Single)
Release Year : 2020
Copyright : (c) 2020
Added By : Huntyr Kelx
Published : Feb 04 , 2020

More TANNAH Lyrics

TANNAH
TANNAH
TANNAH

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl