Wageni Lyrics by PAUL CLEMENT


Katika maisha yangu
Nilipokea wageni
Nikawakaribisha kwangu
Wakafanya vitu vingi
Hawakuwa wa kudumu
Walikuwa wapitaji
Ila moyo wa ukarimu
Ukanisababishia machozi

Mgeni wa kwanza alikuwa ni uchungu
Akaniumiza, akanipa maumivu
Alipomaliza akaenda zake
Mgeni wa pili alikuwa ni huzuni
Huyu naye
Akanikosesha furaha
Mgeni wa tatu alikuwa ni magonjwa
Akanidhoofisha, akataka kuniua
Hakufanikiwa akaenda zake

Aliyefuata alininyima watoto
Jina lake tasa
Naye alipita

Mgeni mmoja jina lake ni mauti
Akamchukua Ntimi, akaniachia jeraha

Mgeni mwingine jina lake hofu
Hakutaka nifanikiwe
Akanipa fikra potofu
Nikajiona siwezi
Tena nitafeli
Huyo naye alipita

Hawa ni wageni
Tena wapitaji
Hawatadumu, watapita
Hawa ni wageni, tena wapitaji
Hawatadumu, watapita

Hakuna jambo lolote gumu
Litakalodumu kwenye maisha yako
Ila yote yatapita
Na yakishapita
Hayatarudi tena

Tough times never last
But tough people do

Mapito siyo mambo magumu unayoyapitia kwenye maisha yako
Ila mapito ni mambo magumu yanayopita kwenye maisha yako
Ndiyo maana ninaita mapito, kwa kuwa yanapita tu
Na yanapita kwenye maisha yako,
Na yakishapita hayawezi kurudi tena, ah

Magonjwa,
Hao ni wageni, tena wapitaji
Hawatadumu, watapita
Uchungu, (Huzuni)
Hao ni wageni, tena wapitaji
Hawatadumu, watapita
Mateso, (Changamoto)
Hao ni wageni, tena wapitaji
Hawatadumu, watapita
(Hata dhiki)
Hao ni wageni, tena wapitaji
Hawatadumu, watapita

Watch Video

About Wageni

Album : Wageni (Single)
Release Year : 2020
Copyright : (c) 2020
Added By : Afrika Lyrics
Published : Jun 03 , 2020

More PAUL CLEMENT Lyrics

PAUL CLEMENT
PAUL CLEMENT
PAUL CLEMENT
PAUL CLEMENT

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl