NACHA Nasimama cover image

Nasimama Lyrics

Nasimama Lyrics by NACHA


Kuna vita skuviona sikuepo enzi zile
Vita vya dunia maji maji Kinjeketile
Vita ya mwafrika na mkoloni niliskiaga
Vita ya Tanganyika na nduli Amin Dada

Tutoke huko tuongelee vita vya sasa
Matumizi ya ubabe kwenye madaraka
Sio vichana wala msiwatukane bure
Wanaposema kuwa ngoma za Nacha zitumike shule

Moyo mchafu kuoshea sabuni
Ni kutegemea ukali wa wembe kuipasua kuni
Kumkosoa boss wako ni kutia mchanga ugali huo
Yaani ni kuning'inia kwenye kamba kuanikia nguo

Nawastaajabu vita vya mamba mnamtegemea kenge
Maana ni nadra sana mbuzi kuzaa mende 
Lahaula maana ni vita sugu
Na mkumbuke kicheko na kilio ni ndugu

Nasimama wima nasimama wima
Na kipima race
Maana umasikini, maradhi ndio vita vya kuogopa
Ujinga kichwani umeshaota 

Haya kamata jembe, kamata shoka 
Shambani ndo utajiri unapotoka
Shika panga na jembe tukasake pembejeo
Tupige vita hivi usipige mkeo

Sina uridhi wa viatu niko peku
Ninafunza nashangaa 
Maana niliskia mcheza kwa hutunzwa
Kuwawashia taa vipofu wasione giza
Ni sawa na kususia uchaguzi sioni tija

La hasha mguji kwenye bukta
Yeye ni hatari ndo hao wanaopeleka sheli buta
Mili mikubwa ila akili hazijakua
Maana mnamtupa samaki kwenye maji ili kumuua

Naishi kwenye vioo chonde msipige mawe
Ukimshindwa adui usione aibu ungana naye
Ndio suruali sio kaptula
Hakuna umoja wenye njaa akitokea mwenye chakula

Wamedukia na walichimba wao kisima
Hawakujua Nuhu wa Shilole sio Nuhu wa safina
Kukosea na ukachukia kutukanwa
Ni kulazimisha kupitisha paka njia za panya

Nasimama wima nasimama wima
Na kipima race
Maana umasikini, maradhi ndio vita vya kuogopa
Ujinga kichwani umeshaota 

Haya kamata jembe, kamata shoka 
Shambani ndo utajiri unapotoka
Shika panga na jembe tukasake pembejeo
Tupige vita hivi usipige mkeo

Kumfuta tongo tongo kipofu alafu useme Yes
Ni sawa na kufosi kumpa jina nameless
Wanaona wivu ila cha ajabu hawaoni haya
Eti uvumilivu na busara pia una expire date

Tulikosea wenyewe but ndugu kuwa wapole 
Mnataka amani ya ndoa na mlioa kwa mtogole
Na vita ni kubwa mtapiga sana miayo
Na msitegemee kushinda kurefa ni kaka yao

Inahitaji akili kuzielewa hizi tungo
Vinginevyo utakunja sura kama mgonjwa wa tumbo
Yaani nampoteza mbwa kwa mingi miluzi
Alafu nashinda kila siku ka na mjomba tume ya uchaguzi

Kupiga vita maadili ni kutoona hayo maboya
Wakati kila siku Insta naona mapaja ya Uwoya
Sasa natoa tamko wakimwagika nawaokota
Nawapanda nawatia mbolea wanaota

Nasimama wima nasimama wima
Na kipima race
Maana umasikini, maradhi ndio vita vya kuogopa
Ujinga kichwani umeshaota 

Haya kamata jembe, kamata shoka 
Shambani ndo utajiri unapotoka
Shika panga na jembe tukasake pembejeo
Tupige vita hivi usipige mkeo

Watch Video

About Nasimama

Album : Nasimama (Single)
Release Year : 2020
Copyright : (c) 2020
Added By : Huntyr Kelx
Published : Sep 17 , 2020

More NACHA Lyrics

NACHA
NACHA
NACHA
NACHA

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl