MAUA SAMA Namwachia cover image

Namwachia Lyrics

Namwachia Lyrics by MAUA SAMA


Yangu furaha, Imegeuka majuto
Kicheko kimegeuka kilio
Ila ninaamini wema hauozi umenipa mazito, me naumia hey
Nilijua  utanifuta machozi umenipa majonzi, me nalia
Zangu hisia nilishindwa kuficha
Wazi wazi ukatambua
Na Ndonga ukanpasua
Wangu rafiki, Wote ulowajua
Na Nguo ukawavua, Pasipo me kujua
Wacha nikae pembeni

(Namwachia Mungu tu)
Labda kuna mahali nilikosea
(Namwachia Mungu tu)
Kesi yako kwake nakushtakia
(Namwachia Mungu tu)
Maana umezidi kunionea
(Namwachia Mungu tu aaaahh)

Nilikupa Muda na vyote vilivyo vyangu
Ila malipo ya yote kunitukanisha na ndugu zangu
Kweli mzoea vya kunyonga vya kuchinja haviwezi
Nimelijua sawa
Moyo wangu umeuchakaza
Umehondomola mpaka gunzi
Wema umenilipa ubaya

Sitoshindwa hata tukionana
Kuachana sio uhasama
Sintothubutu kuzozana nimekunawa
Nakuombea kheri salama
Umpate yule mtakae wezana
Kumbuka kugunga zipu bwana msije kwazana
Zangu hisia nilishindwa kuficha
Wazi wazi ukatambua
Na Ndonga ukanpasua
Wangu rafiki, Wote ulowajua
Na Nguo ukawavua, Pasipo me kujua
Wacha nikae pembeni

(Namwachia Mungu tu)
Labda kuna mahali nilikosea
(Namwachia Mungu tu)
Kesi yako kwake nakushtakia
(Namwachia Mungu tu)
Maana umezidi kunionea
(Namwachia Mungu tu aaaahh)

Watch Video

About Namwachia

Album : Cinema (EP)
Release Year : 2022
Added By : Farida
Published : Jun 08 , 2022

More MAUA SAMA Lyrics

MAUA SAMA
MAUA SAMA
MAUA SAMA
MAUA SAMA

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl