Wosia Lyrics by KALA JEREMIAH


Wanangu sogeeni
Wanangu nina jambo nalotaka waambieni
Muda wangu umetimu wa kuondoka duniani
Nawaachia usia wanangu kapendaneni

Nasisitiza tena wanangu kapendaneni
Ilindeni amani kesheni mkisali
Shetani asiwarubuni fungueni macho yenu
Ili muone ya ndani

Hakika nimetenda Mungu aliyonituma
Nawaombea kwa baba msijekurudi nyuma
Mshikamano wenu gurudumu kusukuma
Msiyumbishe mashua upepo unapovuma

Wosia wako baba unanichoma sana mpaka moyoni
Yale matendo yako nitaishi nayo kwangu rohoni
Hivi kweli unaenda, kweli unaenda, kweli unaenda baba
Hivi kweli unaenda, baba unaenda, kweli unaenda baba

Sasa nazama chini macho yangu juu ya mbingu
Roho inaponyoka mbele naona ukungu
Napita katikati ya uvuli wa mauti
Moyo wangu umechoka na mwili u mahututi
Napigania nafsi na nia ni madhubuti
Naisaka pumzi yangu ya mwisho sauti

Ya malaika wa zamu inanisisitiza
Naona mwanga juu lakini chini ni giza
Mbele yangu nayaona malango ya mbinguni
Niagieni ndugu zangu tutakutana Canaani
Tazama sasa nimezungukwa na ndugu
Mikononi mwako baba naiweka roho yangu

Wosia wako baba unanichoma sana mpaka moyoni
Yale matendo yako nitaishi nayo kwangu rohoni
Hivi kweli unaenda, kweli unaenda, kweli unaenda baba
Hivi kweli unaenda, baba unaenda, kweli unaenda baba

Nimevipiga vita vilivyo vizuri
Mwendo nimeumaliza sasa nakata kauli
Shusheni mwili wangu sasa unataka kaburi
Roho yangu i tayari kwenda masafa ya mbali
Maandiko msipuuze mkajisomee Zaburi
Na nuru iwamulike kama jua la adhuhuri
Andaeni mapito watu wawanenee mazuri
Pandeni mbegu za wema mkajipatie kivuli
Ndani ya moyo wangu nimewaweka muhuri
Nitawapenda mpaka ukamilifu wa dohari
Lindeni muungano ilindeni jamhuri
Tutaonana tena ila kwa sasa kwaheri

Wosia wako baba unanichoma sana mpaka moyoni
Yale matendo yako nitaishi nayo kwangu rohoni
Hivi kweli unaenda, kweli unaenda, kweli unaenda baba
Hivi kweli unaenda, baba unaenda, kweli unaenda baba

 

Watch Video

About Wosia

Album : Wosia (Single)
Release Year : 2021
Copyright : (c) 2021
Added By : Huntyr Kelx
Published : Mar 19 , 2021

More KALA JEREMIAH Lyrics

KALA JEREMIAH
KALA JEREMIAH
KALA JEREMIAH
KALA JEREMIAH

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl