IBRAAH Nani cover image

Nani Lyrics

Nani Lyrics by IBRAAH


(Mocco)

Asubuhi kumekucha 
Wingu limetanda
Na mvua yata kunyesha 
Na uko mbali mama

Maji takitiririka 
Oh baridi itanishika
We ndo chanda chema
Uhakika unanikatisha tamaa

Utaambiwa binadamu
Ah kila mmoja ana mapungufu yake
Sijui nilipoteleza mama

Si ungeniambia
Nimemiss tabasamu
Kutwa kucha 
Picha kummezea mate

Yangu fimbo umeibeza
Ah katu hautaki kuitumia

Labda hesabu za kutoa
Mi niligawanya baby unisamehe
Na ile hasi nikafanya chanya
Baby unisamehe

Na hata emoji za kulia
Nazo kutumia nazo zikome
Japo nipate furaha
Ah huruma unionee

Maana hii hali, hata haifichiki
Kutwa wima cha mpingo, kisiki
Maana hata nikiona michezo ya njiwa
Ah huwa naitamani

Kama si wewe

Nitampenda nani?
Nitampenda nani?
Nitampenda nani
Nani nitampenda 

Nitampenda nani?
Nitampenda nani?
Nitampenda nani
Nani nitampenda aah

Eh penzi usifanye kwa chombo cha usafiri
Ikawa umeshuka uje utanikatili
Nitakuwaga mental Niko dhahari
Si unasikia

Penzi la dhati daima la wawili
We fanya na urudi lisiwe batili
Ka wafanya kusudi ni ukatili
Mi naumia

We ndo yangu hifadhi 
Labda nilikosea msimbo
Kweli kupenda kazi 
Wangu umegeuka fimbo o

Mi ndo lako koroboi
Lile lisilo zima
Aha si ulisemaga hauchomoi
Kumbe imani ulinipima ah

Pia ulisema haudonoi 
Wameiteka mazima
Ahaa simung'unyi sikohoi
Sina vyangu nimechina

Maana hii hali, hata haifichiki
Kutwa wima cha mpingo, kisiki
Maana hata nikiona michezo ya njiwa
Ah huwa naitamani

Kama si wewe

Nitampenda nani?
Nitampenda nani?
Nitampenda nani
Nani nitampenda 

Nitampenda nani?
Nitampenda nani?
Nitampenda nani
Nani nitampenda aah

Watch Video

About Nani

Album : Steps EP / Nani (EP)
Release Year : 2020
Copyright : (c) 2020 Konde Music Worldwide.
Added By : Huntyr Kelx
Published : May 06 , 2020

More IBRAAH Lyrics

IBRAAH
IBRAAH
IBRAAH

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl