FRASHA Wajinga Sisi cover image

Wajinga Sisi Lyrics

Wajinga Sisi Lyrics by FRASHA


Hello, Hello! King Kaka, ni Frasha hapa
Manze hii fight alone hauwezi toboa 
So nimeamua kustand na wewe
So kabla wani-surmone wacha nitoe yangu surmone

Naskia Waiguru amekusue, is this true?
Funny vile judiciary imekuwa circus
Judge na politicians wakiwa main acts
Mshukiwa anaachiliwa kwa bondi ya milioni mbili 
Na kesi yake ni ya bilioni mbili
Nani atatupigania?

Hatujui maguru wa NYS 
Na Ruto na makesi za mashamba scandal za mahindi 
Na story za Mumias na sukari 
Na ata kama we ni pastor unang'ang'anana 
How can you have a deceitful tongue?
But Sunday church bado tutajazana
Wajinga Sisi!

Story ya SGR tuliacha kujicompare na Ethiopia
Wale pia walikuwa wanapiga kelele walinyamazishwa
Pia 'hello unanskia?' 
System ya education ni ya kubebesha punda mzigo 
Hapo ndo mwanzao wa mitego

We go to schools to become educated fools with no jobs
Justice ni ya wenye doh
Lawyers nao ni beneficiaries of failed system
No wonder masomo inaitagwa system, Wajinga Sisi!

Na ata kama wakitumada 
Damu ya Sharon bado Inatu-owe bado 
Siogopi kufa juu kwa system niko dead
Na bado me si sonko

Na hakutakuwa na commission of inquiries
Wasee wapate makazi na salary 
No wonder bado vijana wako moody daily
Wakiworry hii kesho itafika lini 
Juu bado si ni wazee na ni future leaders
Hello, Hello, mnanisikia? Wajinga Sisi!

Daily tuko kwa mitandao IG na Twitter 
Tukionesha venye tunaishi poa 
Ni kama kila mtu alitoboa
Picha kwenye hoteli na meli daily 
But ukweli tuko chini tunasuffer 
Vitu hard kwenye ground

Kwenye matanga hakuna mtu ako sad
Familia ikilia wanasiasa wanaji campaign-ia 
nimesaidia familia na elfu mia 
Kisha makofi tunawapigia
Wajinga Sisi!

Itaanza kutuuma lini sisi? 
Itaanza kutusumbua lini sisi?
Future generations ni kina nani?
Na nani watawapigania 
Tunashinda tukipuliza gunia

Eeeh Mungu nguvu yetu
Ilete baraka kwetu
Haki iwe ngao na mlinzi
Na tukae na undugu, amani na uhuru

Bado kuwa mkenya najivunia
But nimechoka kuvumilia 
Time ni ya kujipigania
Tokeni mitandaoni 
Kujeni tujenge Kenya

Maovu ni maovu
Haijalishi ni nani aliyatenda
Na sitasimama maovu yakitawala
Wakiuza sura badala ya kuuza sera
Ju hand-outs hazitawai kujengea barabara
Hand-outs hazitawai kujengea shule
Hand-outs ndio kabila ya umasikini

Hallo!

Watch Video

About Wajinga Sisi

Album : Wajinga Sisi (Single)
Release Year : 2019
Copyright : (c) 2019
Added By : Huntyr Kelx
Published : Dec 23 , 2019

More FRASHA Lyrics

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl