Paroles de Koroga Par SAIDAN


Umenifisadi kiuchumi waleti umeiacha zero
Ni wewe wewe mwenye macho ya euro
Ulinidanganya msambaa kumbe mchaga wa Kilimanjaro
Unaipenda pesa kama laini na vocha 
Umenifanya ndondocha mi siwazi kukuwacha
Nimedata na penzi maisha majonzi
Mapenzi tulianza juzi unataka nikununulie Benzi
Una mvuto wa ngekewa kujinasua siwezi

Nimesha pata ukweli wewe mi matame 
Tanga ulikuja kwa bibi wazazi wako wanaishi Same
Upendo wako kwangu kungu unaashiria jua kali
Na ndoto za utajiri bora kwako ni jazari
Lakini ninafikiri jinsi fulani nitaja nitajihadhari

Nahisi mami umenichanganya akili
Kwa nguvu za tunduli, kitaa wananijadili
Saidan sieleweki, nishageuka ka jokeli
Zila akili za skuli zote utazikabili
Siwazi lile wala hili nakufuata ka kivuli
Eeeh nakufuata ka kivuli, kwenye mvua mi mwavuli

Maana umenikoroga, umenivuruga
Acha tu nikwambie akili umeichanganya wee
Napata dhoruba nimekuwa rubaa
Yaani kwako nang'ang'ana wee

Umenikoroga, umenivuruga
Acha tu nikwambie akili umeichanganya wee
Napata dhoruba nimekuwa rubaa
Yaani kwako nang'ang'ana wee

Maswali mengi nimejiuliza kichwani
Uliporoga ni Handeni ama Pangani
Nakosa jibu nimebaki kuwa bubu
Huu upendo wa dhati naona unanisulubu
Ukiporoga ni kwa bibi ama kwa babu
Dakika tano nikikumisi nalia ajabu

Kwanini kichwani ndo wazo 
Na naongea na mtu na unakata mazungumzo
Nimezidi kukupenda mpaka inakuwa tatizo
Ukisafiri nabaki tu stendi 
Jua linanichoma mi natekwa na makundi

Upendo gani? Najishangaa
Nyumbani sitoki nilipokaa nimebung'aa
Mapenzi ya dhati hakuna, unanipa kwa mkataba
Sijui ni kipi kilichomfanya nikawa zoba
Umenishawishi nikauza nyumba ya baba
Kwa pressure akafariki sijahudhuria ata msiba
Na ukisema tuachane natamani kujiua
Haki ya Mungu kwa mganga umeniendea 
Na uliporoga mpaka sasa sijapajua 

Umenikoroga, umenivuruga
Acha tu nikwambie akili umeichanganya wee
Napata dhoruba nimekuwa rubaa
Yaani kwako nang'ang'ana wee

Umenikoroga, umenivuruga
Acha tu nikwambie akili umeichanganya wee
Napata dhoruba nimekuwa rubaa
Yaani kwako nang'ang'ana wee

Umenichoma vibaya, baya
Nasurubika sipati dawa
Umenichoma vibaya, baya
Nasurubika sipati dawa

Ecouter

A Propos de "Koroga"

Album : Koroga (Single)
Année de Sortie : 2019
Copyright : (c) 2019
Ajouté par : Huntyr Kelx
Published : Aug 15 , 2019

Plus de Lyrics de SAIDAN

Commentaires ( 0 )

Aucun commentaire pour l'instant



A propos de AfrikaLyrics

Afrika Lyrics est la plus large collection de paroles de chansons et de traductions d’Afrique. Afrika Lyrics fournit les paroles des musiques de plus de 30 pays africains et des traductions de lyrics de plus de 10 langues africaines en français et en anglais.

Suivre Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl