PAPI CLEVER & DORCAS E’ Mungu Mwenye Haki cover image

Paroles de E’ Mungu Mwenye Haki

Paroles de E’ Mungu Mwenye Haki Par PAPI CLEVER & DORCAS


E’ Mungu mwenye haki, uniongoze huku
Katika mambo yote yanayokupendeza
Nikiwa huku bila wewe, vitisho hofu na mashaka
Yananitia tetemeko mpaka kufa
Nikiwa huku bila wewe, vitisho hofu na mashaka
Yananitia tetemeko mpaka kufa

Ni heri siku zote kutegemea Yesu
Na kuenenda sawa katika nyayo zake
Kwa kuwa yeye ni mchunga anayeniongoza vema
Nipate kuingia katika raha yake
Kwa kuwa yeye ni mchunga anayeniongoza vema
Nipate kuingia katika raha yake

Safari yangu sasa yaelekea mbingu
Mwokozi yuko huko, lazima nifikeko
Na siku nitakapofika ‘tashangilia kwa furaha
Kuona yeye aliyeninunua kwake
Na siku nitakapofika ‘tashangilia kwa furaha
Kuona yeye aliyeninunua kwake

Ulimwenguni humu, matata na kuchoka
Nikihitaji kitu nafadhahika bure
Lakini siku ile kuu nita’pomwona Mwokozi
Natumaini sitakosa dhawabu yangu
Lakini siku ile kuu nita’pomwona Mwokozi
Natumaini sitakosa dhawabu yangu

Mbinguni sitaona adui zangu tena
Hayatakuwa mambo yakupokonya pale
Mbinguni sitaona adui zangu tena
Hayatakuwa mambo yakupokonya pale
Sauti nitamtolea, kusema: Mungu, haleluya
Mikono nitaipepea kwa shangwe kuu
Sauti nitamtolea, kusema: Mungu, haleluya
Mikono nitaipepea kwa shangwe kuu

Ecouter

A Propos de "E’ Mungu Mwenye Haki"

Album : E’ Mungu Mwenye Haki (Single)
Année de Sortie : 2023
Ajouté par : Farida
Published : Jul 13 , 2023

Plus de Lyrics de PAPI CLEVER & DORCAS

PAPI CLEVER & DORCAS
PAPI CLEVER & DORCAS

Commentaires ( 0 )

Aucun commentaire pour l'instant



A propos de AfrikaLyrics

Afrika Lyrics est la plus large collection de paroles de chansons et de traductions d’Afrique. Afrika Lyrics fournit les paroles des musiques de plus de 30 pays africains et des traductions de lyrics de plus de 10 langues africaines en français et en anglais.

Suivre Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl