Paroles de Fungu Par LINEX SUNDAY MJEDA


Yaani kufunga na kufungua 
Ukabeba kilicho chako
Umeniongezea maumivu 
Walonionyesha wenzako

Umepepea na furaha 
Ya mtoto wa mwanamke mwenzako
Ukaniweka rahani kisa
Penzi la kunicherehani

Na hata nikijishusha unakuja juu
Imekuwa nongwa unaongea kikuu
Nilisimama kifua mbele kama sina tatizo nawe
Kumbe ninakulia ndani niache nijiishie eeh

Labda haukuwa riziki yangu
Kama na fungu langu ananipokonya
Wacha niyaone mwenyewe
Mbona hata mama ameshanikanya
(Labda alikuwa fungu langu)
(Oooh labda)

Labda haukuwa riziki yangu
Kama na fungu langu ananipokonya
Wacha niyaone mwenyewe
Mbona hata mama ameshanikanya
(Alishanikanya mama sikutaka kusikia)
(Ayayaya)

Penzi limekuwa matapishi 
Linanuka ng'onda
Nilijifanya mbishi
Leo naunguza donda

Mi napalilia mapishi
Wenzangu wanaonja
Maibilisi 
Wazima na wagonjwa

Kama ungeniweka wazi
Mapema tungeachana
Moyo ushakufa ngazi
Kwa kupigwa dana dana

Kutwa nina simanzi
Nishakata taama
Natamani nijitie kitanzi
Nisikuone mama

Nilisimama kifua mbele
Kama sina tatizo nawe
Kumbe naukunia ndani

Kulakoloze kwa vyozevyo, wa ngoze
Kulakoloze chane 

Labda haukuwa riziki yangu
Kama na fungu langu ananipokonya
Wacha niyaone mwenyewe
Mbona hata mama ameshanikanya
(Labda alikuwa fungu langu)
(Oooh labda)

Labda haukuwa riziki yangu
Kama na fungu langu ananipokonya
Wacha niyaone mwenyewe
Mbona hata mama ameshanikanya
(Alishanikanya mama sikutaka kusikia)
(Ayayaya)

Wacha niyaone mwenyewe....

Ecouter

A Propos de "Fungu"

Album : Fungu (Single)
Année de Sortie : 2020
Copyright : (c) 2020 VOA
Ajouté par : Huntyr Kelx
Published : Jan 24 , 2020

Plus de Lyrics de LINEX SUNDAY MJEDA

LINEX SUNDAY MJEDA
LINEX SUNDAY MJEDA
LINEX SUNDAY MJEDA
LINEX SUNDAY MJEDA

Commentaires ( 0 )

Aucun commentaire pour l'instant



A propos de AfrikaLyrics

Afrika Lyrics est la plus large collection de paroles de chansons et de traductions d’Afrique. Afrika Lyrics fournit les paroles des musiques de plus de 30 pays africains et des traductions de lyrics de plus de 10 langues africaines en français et en anglais.

Suivre Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl