Paroles de Jela Par DOGO SILLAH


Daddy naiandika barua 
Nina imani itakufikia
Mi mwanao naumia
Majukumu uloniachia

Mama naye kafariki ee
Wadogo zangu nitawaleaje?
Hata shule nimeshindwa mie
Mawazo kichwani mi nawazaje

Kwanza kosa ni nini daddy
Lilo kufanya uende jela?
Nasikia tu majirani
Wengine wanasema eti uliua

Kama unavyojua, umri wangu mdogo
Mdogo na nategemewa
Majukumu ni mengi
Ni mengi na naelemewa

Daddy ni lini utatoka jela
Uje umwone Khan na Nilima
Leo hatuna hata pa kulala tunaumia  

Daddy ni lini utatoka jela
Uje umwone Khan na Nilima
Leo hatuna hata pa kulala tunaumia 

Sillah, oooh barua yako nimeipata 
Eh eh eh musilie mwanangu (Nyamaza)
Usijali nitatoka (Nyamaza)
Tazama wadogo zako na uwatuze (Nyamaza)

Karibu nitarudi (Nyamaza)
Mwambie jirani yetu Mama Shufa(Nyamaza)
Awape hata uji (Nyamaza)

Na kama mkishindwa nendeni mkaombe ila msiibe
Kimeniumiza sana kifo cha mama yako
Ingawa sijui chanzo ni  nini
Chanzo ni nini

Okey soma mwanangu usiache shule
Soma mwanangu nakutegemea wewe
Mwanangu wee, we ndo kidume
Nakusisitiza ndugu zako watunze

Na kuhusu kosa langu la mi kuwa jela
Ukikuwa utajua
Mtoto wa kiume simba hafundishwi kuwinda
Hivyo najua utashinda

Kwaheri wasalimie wenzako
Waambie nawapenda nitarudi nyumbani
Tuishi kama zamani, zamani

Kama unavyojua, umri wangu mdogo
Mdogo na nategemewa
Majukumu ni mengi
Ni mengi na naelemewa

Daddy ni lini utatoka jela
Uje umwone Khan na Nilima
Leo hatuna hata pa kulala tunaumia  

Daddy ni lini utatoka jela
Uje umwone Khan na Nilima
Leo hatuna hata pa kulala tunaumia 

Sillah, oooh barua yako nimeipata 
Eh eh eh musilie mwanangu (Nyamaza)
Usijali nitatoka (Nyamaza)
Tazama wadogo zako na uwatuze (Nyamaza)

Karibu nitarudi (Nyamaza)
Mwambie jirani yetu Mama Shufa (Nyamaza)
Awape hata uji (Nyamaza)

Ecouter

A Propos de "Jela"

Album : Jela (Single)
Année de Sortie : 2020
Copyright : (c) 2020
Ajouté par : Huntyr Kelx
Published : Jul 11 , 2020

Plus de Lyrics de DOGO SILLAH

DOGO SILLAH
DOGO SILLAH
DOGO SILLAH

Commentaires ( 0 )

Aucun commentaire pour l'instant



A propos de AfrikaLyrics

Afrika Lyrics est la plus large collection de paroles de chansons et de traductions d’Afrique. Afrika Lyrics fournit les paroles des musiques de plus de 30 pays africains et des traductions de lyrics de plus de 10 langues africaines en français et en anglais.

Suivre Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl