BEST NASO Ndoto cover image

Paroles de Ndoto

Paroles de Ndoto Par BEST NASO


Mji siujui jina lake
Mji siijui nchi yake 
Ni kwenye ndoto

Nimekutana naye John Pombe Magufuli
Jana kwenye ndoto (Kwenye ndoto)
Ilikuwa kwenye mji wa kifahari
Mji wenye vingi vyote vizuri

Ooh mara napita naskia nimeitwa
Tena na sauti ambayo naikumbuka
Nikamwona John Pombe nikahisi furaha
Ameketi pazuri pa kifahari, ooh John
Akanikaribisha na neno zuri la kuchekesha
Akauliza, akauliza vipi kuhusu Tanzania yangu
Unamwonaje mama Samia, ulivyoondoka mzee amezushwa mengi
Kama uijuavyo Bongo (Bongo)

Jakaya mzee Kinena walizushiwa wamekuua
Ni nani alisambaza upuzi huo
Kifo changu asihusishwe mtu yeyote
Mimi nilikuwa na maradhi yaliyokuwa yananisumbua
Kwa muda mrefu kidogo, na muda umefika Mungu amenichukua
Ukweli unabaki ukweli

Mzee Tanzania imekumiss, tena imemiss ile mikiki mikiki
Mzee ile siku ya kifo chako ulichanganya kifo sana
Afande Sele bila uoga akamtukana Mungu akakufuru
Kuna wengine waliokuja kukuaga uwanja wa Taifa wakafa (Johnny)
Wale wamama uliokuwa unawatetea walisikia matoki imeingia

Ndugu zangu nawapa pole sana
Na vipi kuhusu mama Samia anaeneza vizuri mikakati yangu
Ndivyo mama Samia tena anapendwa kweli kweli
Ila tatizo ni mpole sana mama

Na nimesikia baada ya kifo changu kuna watu wamenisaliti
Mzee ndivyo dunia tambara mbovu
Hata ufanye vipi ukasifiwa
Ukifa huwezi kosa msaliti

Huo ni ukweli kijana wangu
Tena ukweli wa Mungu
Na vipi kuhusu mama Janet Mke wangu 
Wanamtunza au?

Ooh mama Janet hali yake haielezeki
Ila ndio hivyo imebidi Mungu kakupenda hana budi
Unajua nilikuwa napenda sana kamziki
Vipi kuhusu Alikiba, Diamond na kijana wangu Harmonize

Mzee game imechangamka ingawa vibeef ndo zinaamka 
Sasa kwa nini usiwashauri vijana wenzako wabadilike
Waache mabeef 
Mzee watu wana vichwa ngumu yaani kama vile wanavuta bangi
Na kuhusu baba Levo na H Baba
Mzee utaniingiza kwenye ugomvi
Chonde chonde mzee hao siwawezi

Nimekuelewa sasa nakupa maaagizo upeleke
Mwambie mama Samia namwamini kweli kweli
Najua mama Samia ni chuma kweli kweli
Tumefanya naye kazi awamu ya tano
Sijaona tatizo lolote kwake
Na naamini atakwenda kufanya mambo mazuri
Ya kuwafurahisha waTanzania

Lakini jambo kubwa mwambie
Ukitaka kumuua nyani usimwangalie usoni
Muda mwingine awe mkali
Mara eeh nikashtuka ndoto
(Moja Moja Records)

 

Ecouter

A Propos de "Ndoto"

Album : Ndoto (Single)
Année de Sortie : 2021
Copyright : (c) 2021
Ajouté par : Huntyr Kelx
Published : Jun 29 , 2021

Plus de Lyrics de BEST NASO

BEST NASO
BEST NASO
BEST NASO

Commentaires ( 0 )

Aucun commentaire pour l'instant



A propos de AfrikaLyrics

Afrika Lyrics est la plus large collection de paroles de chansons et de traductions d’Afrique. Afrika Lyrics fournit les paroles des musiques de plus de 30 pays africains et des traductions de lyrics de plus de 10 langues africaines en français et en anglais.

Suivre Afrika Lyrics

© 2025, We Tell Africa Group Sarl