A patriotic song by Eric Wainaina 

...

Daima Mkenya Lyrics by ERIC WAINAINA


Umoja ni fahari yetu
Undugu ndio nguvu
Chuki na ukabila
Hatutaki hata kamwe
Lazima tuungane, tuijenge nchi yetu
Pasiwe hata mmoja
Anaetenganisha

Naishi, natumaini
Najitolea daima Kenya
Hakika ya bendera
Ni uthabiti wangu

Nyeusi ya wananchi na nyekundu ni ya damu
Kijani ni ya ardhi, nyeupe ya amani
Daima mimi mkenya
Mwananchi mzalendo

Kwa uchungu na mateso
Kwa vilio na huzuni
Tulinyakuliwa Uhuru
Na mashujaa wa zamani
Hawakushtushwa na risasi
Au kufungwa gerezani
Nia yao ukombozi
Kuvunja pingu za ukoloni

Naishi, natumaini
Najitolea daima Kenya
Hakika ya bendera
Ni uthabiti wangu

Nyeusi ya wananchi na nyekundu ni ya damu
Kijani ni ya ardhi, nyeupe ya amani
Daima mimi mkenya
Mwananchi mzalendo

Wajibu wetu
Ni Kuishi kwa upendo
Kutoka ziwa mpaka pwani
Kaskazini na kusini

Naishi, natumaini
Najitolea daima Kenya
Hakika ya bendera
Ni uthabiti wangu

Nyeusi ya wananchi na nyekundu ni ya damu
Kijani ni ya ardhi, nyeupe ya amani
Daima mimi mkenya
Mwananchi mzalendo

Kijani ni ya ardhi, nyeupe ya amani
Daima mimi mkenya
Mwananchi mzalendo

Watch Video

About Daima Mkenya

Album : Daima Mkenya (Single)
Release Year : 2015
Copyright : (c) 2020
Added By : Huntyr Kelx
Published : Oct 20 , 2020

More ERIC WAINAINA Lyrics

ERIC WAINAINA
ERIC WAINAINA
ERIC WAINAINA

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl