BWANA MISOSI Mungu Yuko Bize cover image

Mungu Yuko Bize Lyrics

Mungu Yuko Bize Lyrics by BWANA MISOSI


Aliumba mbingu nchi na bahari
Aliumba samaki pori wanyama wakali
Milima nyota mwezi mchana na juakali
Apewe sifa utukufu wala sikitendawili
Alimuumba dume adamu fahari
Akamuumba jike pia eva wake mwali
Akaleta ndoa ili waoane
Akasema kazi imebaki sasa mzaane
Hii hadithi ya kweli ya jana kama ya kesho
Alizaliwa abeli kaini musa na petro
Binadam unajifanya kwamba uko bize
Bize kuliko mungu alieumba bize
Aliumba mchana nabado akaleta mkesha
Akashuhudia vita akazikomesha
Ukamuomba akuponye na ukapona presha
Ukatengeneza gari leo unaliendesha
Mungu wa wamasai mungu wa mang’ati
Aliemfanya daudi mshinde goriati
Alimuumba na osama binladen miaka ya kati
Akamfanya huyu bwana asomee juu ya dawati
Anafanya dunia nzima iwe na umoja
Ili isiwe kama septemba kumi ma moja
Hana mfano kumsujudu kumuabudu kumtukuza
Peke ake kwamba yeye ndio muweza
Mengi amefanya nab ado miaka imekatika
Hajasema sasa basi minapumzika
Kaenda Kenya na Zimbabwe kwa samba wa nyika
Mugabe shangirai kibaki odinga washirika
Alimuumba rushahu akamzaa joseph
Akamuumba shabani akamzaa sefu
Aliuumba msamaha na akasamehe wakosefu
Nikipi unachofanya matendo masafi au machafu

Kila kitu unachofanya (unachofanya)
Mungu yuko bize zaidi yako
Kila kitu unachofanya (unachofanya)
Mungu yuko bize zaidi yako
Bizeee eeeeehh
Mungu yuko bize zaidi yako
Bizeee eeeeehh
Mungu yuko bize zaidi yako

Hii ni bize ya mungu ndugu isome kwa vina
Ubavu kibao kampa braza johnsiner
Kawapa vipaji ndugu venas na serena
Kawapa macho madogo wajapan na wachina
Kamuumba bruce lee akafa na jina
Kamuumba fagason kwa wale wapenzi wamanchesta
Kamuumba gaucho chuji bonan na ngasa
Kafanya taifa star kwasasa inakubalika
Kafanya bongo uchaguzi uwe na amani
Kamuweka zitokabwe katiba ramani
Kampa kikwete uenyekiti wa afrika
Kaipa nyumbani kigoma ziwa Tanganyika
Kafanya Obama ameika anakubarika
Huyu mungu wa ajabu mwenye kutawala naimba
Hajawahi kusinzia hajawahi kulala
Yuko bize zaidi ya bizebize kila idara
Kuna walemavu wazima wanamuonba yeye
Pia majambazi wachamungu wanamuomba yeye
Baraka za wote zitoke kwake yeye
Nani yuko bize nauliza zaidi ya yeye
Kuna wakristo huku kuna waislam
Kuna wachungaji huku kuna mahimamu
Bado kuna pepo huku jehanamu
Umekosa leo labda tomorrow ndio yako zamu
Kamuongoza zuma south afrika amekubalika
Kawapa naijeria psuare na 2face
Braza chacha na ditopile wamekufa na tetesi
Lakini kwa mungu yote hayo bado mepesi
Kanyongwa mtu maarufu sadam ameshuhudia
Yameundwa mabom kibao tu ya n’yukilia
Bado mungu anaisimamia
Kazi yake kubwa kuiponya hii dunia

Kila kitu unachofanya (unachofanya)
Mungu yuko bize zaidi yako
Kila kitu unachofanya (unachofanya)
Mungu yuko bize zaidi yako
Bizeee eeeeehh
Mungu yuko bize zaidi yako
Bizeee eeeeehh
Mungu yuko bize zaidi yako
Kila kitu unachofanya (unachofanya)
Mungu yuko bize zaidi yako
Kila kitu unachofanya (unachofanya)
Mungu yuko bize zaidi yako
Bizeee eeeeehh
Mungu yuko bize zaidi yako
Bizeee eeeeehh
Mungu yuko bize zaidi yako

Watch Video

About Mungu Yuko Bize

Album : Mungu Yuko Bize (Single)
Release Year : 2022
Added By : Farida
Published : Sep 15 , 2022

More BWANA MISOSI Lyrics

BWANA MISOSI

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl