Ujana Lyrics by ASALA


Kweli mapenzi ushujaa 
Vita ni kupambana
Yule anaye kupenda sana
Ndo utamuona yeye ana maana

Ngoja nikwambie
Kupendwa bahati wanatafuta wenzako
Tena usikie
Hairudi mara mbili tumia nafasi yako

Nafsi imejawa tamaa
Macho yanakutazama
Vyomoni nakupenda sana 
Kumbe moyoni nakudanganya

Tatizo lako wewe
Kila kitu unakitaka wewe
Dunia ina wengi we
Hutaweza kumaliza utamu wee

Kila kukicha nafadhaika 
Kaka eeh
Moyo hutaki ridhika
Mpaka nimpate Wema eeh

We mwana ukome tena domo lishone
Naona kama unavuka mipaka
Usijidanganye na usijichanganye
Kashindwa simba utaweza wewe paka

Si unajuaga ujana
Una mambo mengi ujana
Chunga sana ujana
Ni maji ya moto ujana

Nasema si unajuaga ujana
Unafanya nisilale ujana
Utalia ujana
Utakupoteza ujana

Mapenzi starehe yangu
Kuwacha siwezi aiyaa
Nazunguka na moyo wangu
Ila pesa ndo nawagawia

Anacheza na akili yako
Ana nguvu sana huyo shetani
Tafuta chaguo lako
Umveshe pete umweke ndani

Dunia ya leo,
Maradhi yako wazi wazi
Achana na vileo
Umaarufu usikupe uchizi

Kila kukicha nafadhaika 
Kaka eeh
Moyo hutaki ridhika
Mpaka nimpate Wema eeh

We mwana ukome tena domo lishone
Naona kama unavuka mipaka
Usijidanganye na usijichanganye
Kashindwa simba utaweza wewe paka

Si unajuaga ujana
Una mambo mengi ujana
Chunga sana ujana
Ni maji ya moto ujana

Nasema si unajuaga ujana
Unafanya nisilale ujana
Utalia ujana
Utakupoteza ujana

Big Sound Music

Watch Video

About Ujana

Album : Ujana (Single)
Release Year : 2019
Copyright : (c) 2019
Added By : Huntyr Kelx
Published : Aug 13 , 2019

More ASALA Lyrics

ASALA

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl