ANAYA Wapo (Cover) cover image

Wapo (Cover) Lyrics

Wapo (Cover) Lyrics by ANAYA


Hivi kwanini nijitutumue
Na dunia sio makazi
Vijineno neno vinisumbue
Hadi nishindwe kufanya kazi

Mama alisema mkuku kwa nguruwe
Kuishi na watu kazi
Achambe atukane ata aniue
Nishasamehe mzazi ni mzazi

Mwenzenu naficha naficha
Mengi ninayoyaona
Kifupi nafunika kombe
Nikiamini kesho nayo siku

Mapicha picha mapicha
Sidhani kama nitapona
Wanangu wa mtaani mniombee
Hii vita ni mchana na usiku

Oooh kuna watu na viatu
Wanatamani milele wawe wao
Ukijituma watasema
Unashinda nao

Oooh ni kama watu
Kumbe ndani wana roho za chatu
Hawatosheki na vikubwa vyao
Wanatamani hata kidogo chako kiwe chao

Mola nipe ujasiri
Kwenye kufanya maamuzi
Zidi nikomaza akili
Isinipoteze miluzi

Uniamshe alfajiri
Kama jana na juzi
Kupata kukosa ni siri
Nawe ndo Mungu Baba mwamuzi

Dear Lord, wapo
Iyeiye iye, wapo
Japo ni ngumu kuwaona, wapo
Wasotaka ufanikiwe

Binadamu hawana jeru, wapo
Kila utachofanya watasema
Nah nah nah nah mmmh

Watakuita mwanga kibonge
Tena kwa dharau wakucheke
Wanachotaka waongee
Waseme shukrani ya punda mateke

Kama vipi dem wake tumgongee
Ndo anayempiga chura teke
Usipoonewa ndonge
Basi ndo ujue hauna makeke

Sikia Konde we pambana mjini shule
Ukipata kidogo letana nao tule
Wachana nao wamesemaga umezoea vya bure
Maana siku zote nyani halioni kundule

Kama baba na mama ndo nguzo ya dunia
Wapende wote
Sio wa kike anacheka wa kiume analialia
Bila msaada wowote

Oooh kuna watu na viatu
Wanatamani milele wawe wao
Ukijituma watasema
Unashinda nao

Oooh ni kama watu
Wana roho za chatu
Hawatosheki na vikubwa vyao
Wanatamani hata kidogo chako kiwe chao

Mola nipe ujasiri
Kwenye kufanya maamuzi
Zidi nikomaza akili
Isinipoteze miluzi

Uniamshe alfajiri
Kama jana na juzi
Kupata kukosa ni siri
Nawe ndo Mungu baba mwamuzi

Dear Lord, wapo
Iyeiye iye, wapo
Japo ni ngumu kuwaona, wapo
Wasotaka ufanikiwe eeh

Binadamu hawana jeru, wapo
Kila utachofanya watasema

Watch Video

About Wapo (Cover)

Album : Wapo (Cover) (Single)
Release Year : 2021
Copyright : (c) 2021
Added By : Huntyr Kelx
Published : Jan 05 , 2021

More ANAYA Lyrics

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl