SERRO Ya Dunia cover image

Ya Dunia Lyrics

Ya Dunia Lyrics by SERRO


Hayeye!
Nimesota, sina wera, juzi nilikopa nilipe mama mboga
Hawajui, hawata amini, juu mi ni mwana mziki na mambo yangu iko fiti
Na huko instagrama, wanadhani nimeosa
Sababu waliona nikikula na Obama

Wengi ni mastar kwa vile wanavyo vaa
Lakini utashangaa, vile wanavyokaa
Wengi hujifanya mambo yao yako sawa
Lakini utashangaa, ni mengi haya ya dunia

Hayeye!
Chakula githeri chemsha na avocado
Na nina deni ya soo mbili ya mama Wambo,
Sasa nasaka fare anagalau nifike show.
Lakini jana si nilikua kwa TV, na juzi pia nilikua kwa gazeti,
Mambo yangu yanafaa kua fiti
Huko instagrama, wanadhani niko poa
Sababu waliona, ile poster ya Koroga

Wengi ni mastar kwa vile wanavyo vaa
Lakini utashangaa, vile wanavyokaa
Wengi hujifanya mambo yao yako sawa
Lakini utashangaa, ni mengi haya ya dunia

Sio yote yang’aayo ni dhahabu,
Watu huficha masaibu kwa tabasamu
Basi sote tuwe wakarimu
Sababu yote yang’aayo si dhahabu

Wengi ni mastar kwa vile wanavyo vaa
Lakini utashangaa, vile wanavyokaa
Wengi hujifanya mambo yao yako sawa
Lakini utashangaa, ni mengi haya ya dunia

Watch Video

About Ya Dunia

Album : Ya Dunia (Single)
Release Year : 2019
Copyright : All rights to the owner.
Added By : Huntyr Kelx
Published : May 09 , 2019

More SERRO Lyrics

SERRO
SERRO
SERRO

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl