Tanzanian Bongo Records artist, Rapcha features Lady JayDee on "AMEN" a new gospel...

Amen Lyrics by RAPCHA


Uh hebu tazameni
Matendo ya Mungu yanavyotisha
Amefanya mengi makubwa ya kustaajabisha
Marafiki leo wana upendo kesho umekwisha
Ila upendo wa Mungu hauwezi kwisha

Naamini neno lako linaishi forever
Utendawazi hauwezi kubadili 
Dhambi ikawa haki, Never!
Umenifikisha sehemu ambazo 
Wala sikuwahi kuzifikiria
Sifa zako nitazihadithia

Unaniepusha na maadui
Unanilinda na mabaya
Ambayo hata siyatambui
Mungu uliye hai
Hata mimba zilizotokea
Kwenye mazingira ya dhambi 
Watoto umewapa uhai

Na kama pumzi unanipa bure
Sasa kivipi tamaa ya pesa initenge na wewe
Nashukuru kwa kunileta hii sayari
Milele nitakuamini Mungu wa kweli AMINA

Amen Baba, Amen
Upendo wako, huruma yako Amen
Wema wako utukufu wako, Amen
Amen Baba, Amen

Umenipa maarifa, umenipa uhai, umenipa mali 
Hata nacho kipaji siwezi sema sijaridhika
Umenipa kile ulichonipa, hukunitupa
Nami sitakijuta Baba, nasema AMEN

Glory to God, utajiri mkubwa ni furaha
Mungu anaweza kubariki mpaka ukashangaa
Niwapo kwenye njaa nikumbushe kwamba
Ndege hawalimi, hawavuni ila hawakosi chochote

Nilipotoka usiwache nikumbusha
Nipe hekima nisitamani magari 
Nisiyoweza kuyaendesha
Niishi kwenye ukweli nidumu
Maana uwongo hauishi milele 
Na unaua faster kuliko sumu

Pia asante kwa kunipa bidii
Napokuomba haujibu haraka
Unajibu wakati sahihi
Una hekima inayoshangaza dunia
Watu hata tungombane vipi
Tunashare mvua na jua

Nilijalie nisilewe sifa
Nikumbuke siku za uhai wangu zinahesabika
Hivyo nikuabudu nikiwa kijana
Nawe utaniweka juu kwa baraka leo zaidi ya jana

Amen Baba, Amen
Upendo wako, huruma yako Amen
Wema wako utukufu wako, Amen
Amen Baba, Amen

Watch Video

About Amen

Album : Amen (Single)
Release Year : 2020
Copyright : (c) 2020 Bongo Records.
Added By : Huntyr Kelx
Published : Jul 18 , 2020

More RAPCHA Lyrics

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl