NACHA Hodi cover image

Hodi Lyrics

Hodi Lyrics by NACHA


Hodi wenyewe Nacha ndo nagonga
Namuulizia ndoa hivi nimemkuta au katoka
Ala kumbe yupo mwite namhitaji huku
Naitaka sana ndoa ila tatizo najishuku

Nataka kujua pia nimekuja kukuuliza
Na kama ndoa ni tamu ni kwanini inawaliza?
Ni kwanini inawaumiza bado najiuliza
Na ni kwanini baada ya ndoa majuto hupitiliza
Wanandoa wengi hawana furaha 
Na wengi wao mara nyingi tunakutana sana bar
Nakata tamaa jirani kila siku zogo
Na na mbona wanandoa wengi wana nyumba ndogo?

Kipi ni sababu ya wanandoa kugombana?
Kitandani hana kipya kwaiyo hana tena maana?
Aliamua kukuigizia na kuwa kakupenda sana
Au mlikurupuka kipindi cha uchumba nyinyi mkaoana

Inanipa wasi inaniwia vigumu
Kuamini nikioa ndoa yangu inaweza dumu
Mawazo yananikumba nikiwaza kuingia ndoa
Nachohofia ni kuingia ule mlango wa kutoka

Hata maji ya moto kuna muda yanapoa
Hakuna kitu kibaya kama kukosea kuoa
Sorry kwa usumbufu ila nilitaka tu nipime
Nitarudi tena wacha nigonge hodi kwingine

I'm coming home 
Nakuja nilivyo, kichwani kiulizo
Coming home, waambie
Milango yote inanikataa 
Acha nijaribu siasa majitaka taka
Dini kabisa hofu napata pata
Ndoa kabisa imenikataa

Ngoja nigonge mlango wa dini nitatue haya mafumnbo
Nijue kinagaubaga sitaki kufuata mkumbo
Mi sio Isaka, Yakobpo wala Musa mwenye fimbo
Wanafanya kwa faida ya Mungu au faida ya matumbo?

Nijitie mkosi na nijisahau
Na mwisho nikapige goti chini mbele ya madhabahu
Au nijivike ugaidi ukaidi hayawani
Au niwe na busara kama mfalme Suleimani

Mlango nyeti hadi kuingia tu naogopa
Mnanishauri niji Macca au mchungaji wa kuokoka
Nikiingia huku kuna vitu nitavikosa
Starehe za kidunia unadhani wapi nitapata?

Mmenipata? Na nacho ogopa 
Ni kumjaribu Mungu kwa kuingia na kutoka
Nimkane kama Petro nimsaliti kama Yudah
Niutangaze ufalme wa Mungu mbele yao nikiwa shuhuda

Niingie kupata pesa 'NO' moto utanichoma
Au niingie kuitangaza injili kila kona
Toa ndugu toa, toa ulichonacho
Ninunue Prado mpya nongeze kipato

Ogopa kuwa Mungu wakati we mwenyewe una Mungu
Siku Mungu akikasirika dunia utaiona chungu
Kuabudiwa kama Mungu na unajua we sio Mungu
Ni kutafuta mchawi nani na unajua mchawi ndugu

I'm coming home 
Nakuja nilivyo, kichwani kiulizo
Coming home, waambie
Milango yote inanikataa 
Acha nijaribu siasa majitaka taka
Dini kabisa hofu napata pata
Ndoa kabisa imenikataa

Kila mlango ni mgumu sioni pakukimbilia
Najiuliza kwanin ni lazima ndani mi kuingia
Kabla sija ghairi nakuna kichwa faster
Nawaza nikagonge labda mlango wa siasa

Naskia ni mchezo mchafu sitaiweza mi ni msafi
Naogopa kulaghai watu mwisho wakipati
Naogopa tega ndoano niwavue hawa samaki
Na mwisho nishibe mimi niwanyime wao haki

Au niingie huenda naeza kuwa bora ka Nyerere
Bora ka Mandela nifikishe nchi mbele
Nikifa nikazikwe kwa shujaa Butiama
Au kaburi langu likazikwe Nyasubi Kahama

Kabla sijaingia kuna vingi niliona
Kura za haki bao la mkono Maradona
Kwa Mungu sasa nitachosema nini?
Ikiwa nilikula nikasaza nikasahau walio chini

Siasa ina makali kama kisu
Nikikumbuka alivyotakaga kuuawa
Nafikiria kutekana nafikiria kuchafuana
Na ndicho naogopa sana

I'm coming home 
Nakuja nilivyo, kichwani kiulizo
Coming home, waambie
Milango yote inanikataa 
Acha nijaribu siasa majitaka taka
Dini kabisa hofu napata pata
Ndoa kabisa imenikataa

Watch Video

About Hodi

Album : Hodi (Single)
Release Year : 2020
Copyright : (c) 2020
Added By : Huntyr Kelx
Published : Apr 16 , 2020

More NACHA Lyrics

NACHA
NACHA
NACHA
NACHA

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl