Tuvushe Lyrics by HARMONIZE


Taifa limeishapata suluhu
Kinachofata ni mipango na
Majaliwa ya mwenyezi Mungu

Analilipanga Mungu huwezi kulipangua
Alitupa Magufuli kisha akamchukua
Amekuachia jahazi na sisi ndio abiria
Jukumu letu ni kuchapa kazi
Maana yupo wa kusimamia

Tutumbulie majambazi 
Wala rushwa na maharamia
Wasiotaka kufanya kazi 
Wapenda pesa za kuvizia

Mama tuvushe
Taifa zima lina imani na wewe (Tuvushe)
Hayati JPM alikuteuwa wewe (Mama Samia tuvushe)
Taifa zima tunakutazama wewee
Mamaa (tuvushe)

Eeh Refarii ndio kabadilika
Lakini uwanja ni ulele
Kazi juu ya kazi

Tena mpenda haki mtu wa Mungu
Fitna hataki wala majungu
Eee na ndoto za wanawake shupavu zimetipia
Na huyu ndio rais wa kwanza mwanamke hapa Tanzania
Mama Samia, anakwenda kumalizia
Miradi iyobakia
Pole yenu mnaoofia

Aaah mamaa waonyeshe unavyotekeleza
Usisi, bigi na serenda madaraja yote
Aa Mamaa Waonyeshe Unavyotekeleza
Na fly-over zilizobakiaa
Mamaa Waonyeshe Unavyotekeleza
Standard gauge, Air Tanzania
Mamaa waonyeshe unavyotekeleza

Mabarabara, elimu bure pia
Mamaa waonyeshe unavyotekeleza
Mradi wa umeme bwawa la nyerere
Mamaa waonyeshe unavyotekeleza
Ikulu chamwino Dodoma izidi songa mbele
Mamaa waonyeshe unavyotekeleza

Watch Video

About Tuvushe

Album : Tuvushe (Single)
Release Year : 2021
Copyright : (c) 2021 Konde Music Worldwide.
Added By : Huntyr Kelx
Published : Jun 12 , 2021

More HARMONIZE Lyrics

HARMONIZE
HARMONIZE
HARMONIZE
HARMONIZE

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl