Utoshefu Lyrics by AMBWENE MWASONGWE


Nimejifunza kuwa radhi, katika hali yeyote niliyonayo
Najua kudhiriwa, tena na kufanikiwa katika hali yeyote
Na katika mambo yeyote nimejifunza kushiba na kuona njaa
Nimejifunza kuwa na vingi na kupungukiwa, nayaweza yote kwa anitiaye nguvu
Utauwa, na kuridhika vimenipa utoshefu
Utauwa, na kuridhika vimenipa utoshefu

Furahini siku zote katika bwana
Tena nasema ndugu zangu furahini
Upole wenu ujulikane na watu wote
Bwana yu karibu kuja
Furaha niliyonayo, ni tunda la roho furaha hiyo hailetwi na vitu
Sisubiri nipewe ili nifurahi, nafurahi hata kwenye mateso
Upole nilionao, umetoka kwa roho hautegemei ninavyotendewa
Amani ya Kristo imenitawala ndani naimba wimbo wakati wa shida
Imenihifadhi moyo na nia yangu ninayapenda mambo ya staha
Haki, usafi kupendeza na sifa njema
Ukiwepo wema wowote nautafakari, nafurahi
Nimehuishwa fikra zangu, nafurahi
Nimeridhika na utauwa kwa bwana

Upendo wa dunia hii una sababu
Sababu hizo zikiisha huisha
Upendo huo ni wa nipe nikupe
Vitu vikienda na upendo umeenda
Furaha ya dunia hii ni ya sababu
Ukivikosa vitu inaisha
Amani ya dunia hii ni ya sababu
Hetengenezwa na mazingira yasiyodumu
Utauwa, na kuridhika vimenipa utoshefu
Utauwa, na kuridhika vimenipa utoshefu
Utauwa, na kuridhika vimenipa utoshefu
Utauwa, na kuridhika vimenipa utoshefu

Nitawapenda watu tena nitawaamini
Ntakupenda zaidi wewe usiyeumiza
Nitafurahi tena nitatabasamu na kuwainyesha mwanya ila sitawapa moyo
Moyo hadanganya
Nitaukabidhi kukupa wewe uliyeuumba, moyo huua
Sitalpa mtu maana haujui
Watu wanatibu ila wewe waponya, wao hunenepesha ila wewe unawandisha
Japo twaanguka twaumia, twateseka tunalia
Wewe bwana ni faraja yetu, nimeridhika
Na utauwa umenipa kutosheka, nimeridhika
Nimekupa moyo wangu utawale
Nimejifunza kuwa radhi, katika hali yeyote niliyonayo
Najua kudhiriwa tena  na kufanikiwa katika hali yeyote
Na katika mambo yeyote nimejifunza kushiba na kuona njaa
Nimejifunza kuwa na vingi na kupungukiwa
Nayaweza yote kwa anitiaye nguvu
Nimejifunza kuwa radhi katika hali yeyote niliyonayo
Najua kudhiriwa tena  na kufanikiwa katika hali yeyote
Na katika mambo yeyote nimejifunza kushiba na kuona njaa
Nimejifunza kuwa na vingi na kupungukiwa
Nayaweza yote kwa anitiaye nguvu

Watch Video

About Utoshefu

Album : Utoshefu (Single)
Release Year : 2021
Added By : Farida
Published : Nov 01 , 2021

More AMBWENE MWASONGWE Lyrics

AMBWENE MWASONGWE
AMBWENE MWASONGWE
AMBWENE MWASONGWE
AMBWENE MWASONGWE

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl