Itakuwaje (Corona) Lyrics by LINEX


Nashauriwa na wataalamu 
Hata mikono yangu mwenyewe
Nisiwe na imani nayo

Kabla ya Corona kuna HIV
Malaria Ebola na mengineyo
Je utamudu maisha kukaa ndani 
Tusiende kazini

Au ndo zama za miaka elfu moja 
Ya utawala wa shetani
Muulize Mungu wako 
Kama kweli ni haki?

Tupunguze kesi za Corona mtaa
Tuanze kuhesabu wangapi 
Wanakufa kwa njaa majumbani
Wataishije wasanii bila makongamano
Au waliopo karantini kwa 14 days
Watavichanga watupe show

[Chorus: Mimi Mars]
Nimefunga sali kwa ajili ya dunia
Na taifa lako 
Hakuna chenye mwanzo kisicho na mwisho
Pesa haina tena dhamani
Watu wanalilia uhai

[Stamina]
Ah yeah naongea na wewe mr Covid 19, Corona
Mzee wa kuweka watu karantin
Nina familia inayonitegemea mimi
Sasa nikikaa ndani watoto watakula nini?

Mbona Ebola hakututesa kama wewe
Daily tupo na malaria na hatutishi kama wewe
Wewe ni nani mpaka uitese dunia?
Nikiviona vifo vyatajwa ndio kabisa huwa nalia

Hebu nenda na please naomba usirudi tena
Usije tena -- ebu tuwache vyema
Mungu ibariki Tanzania hili nalo litapita
Mungu ibariki dunia 

[Chorus: Mimi Mars]
Nimefunga sali kwa ajili ya dunia
Na taifa lako 
Hakuna chenye mwanzo kisicho na mwisho
Pesa haina tena dhamani
Watu wanalilia uhai

[Belle 9]
Halina suluhisho hili tatizo
Tusali kwa imani majumbani
Ee Mungu baba tuokoe
Nawaza na wenzangu na mimi
Wale wenye hali za chini
Riziki zao nnje ya mlango
Wafuate mpango, nani atawaletea

[Country Boy]
Hey Corona please I'm talking to you
Unataka nini -- I know what to do
Wtf you came from? umetokea hatuvijui
Kasi haiendi kifupi maisha taabu tu
So we pray to God na hili lipite
Tuwe makini tujilinde ili tusijizike
Watoto wa kiume na kike taarifa zifike
Kaa nyumbani wash your hands alafu msikusanyike

[Chorus: Mimi Mars]
Nimefunga sali kwa ajili ya dunia
Na taifa lako 
Hakuna chenye mwanzo kisicho na mwisho
Pesa haina tena dhamani
Watu wanalilia uhai

[Belle 9]
Nawaza na wenzangu na mimi
Wale wenye hali za chini
Riziki zao nnje ya mlango
Wafuate mpango, nani atawaletea

Dunia inasikitika
Machozi yanatutoka
Wagonjwa wanaongezeka 
Tiba wapi umefichwa
Dunia inasikitika

[Linex]
Ni kweli Mungu hamtupi mja wake
Lakini kinga ni bora kuliko tiba
Tuyafuate maelekezo 
Tunayopewa na wizara ya afya
Tuyafuate maelekezo 
Tunayopewa na wizara ya afya

(Itakuwaje?)

[Chorus: Mimi Mars]
Nimefunga sali kwa ajili ya dunia
Na taifa lako 
Hakuna chenye mwanzo kisicho na mwisho
Pesa haina tena dhamani
Watu wanalilia uhai

Watch Video

About Itakuwaje (Corona)

Album : Itakuwaje (Corona) (Album)
Release Year : 2020
Copyright : (c) 2020 The VOA.
Added By : Huntyr Kelx
Published : Apr 13 , 2020

More LINEX Lyrics

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl